Wakaazi wa mtaa wa Kangemi hapa jiji Nairobi leo wamewauwa kwa kuwateketeza moto majambazi watatu waliokuwa katika harakati za kutekeleza wizi katika eneo hilo.
Thursday, May 23, 2013
Consortium of NGOs takes Loliondo matter to Kikwete
By MASEMBE TAMBWE
An international consortium of local communities, indigenous peoples and NGOs (ICCA) has raised its concern with the government about the proposed Loliondo Game Controlled Area division, saying the move will threaten both conservation and local livelihood interests.

President Jakaya Kikwete
According to a statement issued by the consortium, a letter has been written to President Jakaya Kikwete and the Minister for Natural Resources and Tourism expressing their deep concern about hiving 1,500 km square of disputed land from community access.
“This could only have a major negative effect on local livelihoods and social well-being. It could create a serious and lasting impediment to sustainable conservation practices in the broader Serengeti region,” the letter stated.
The ICCA consortium promotes global recognition of, and support for, areas conserved by indigenous peoples and local communities.
It is a partner organization of the Convention on Biological Diversity, the United Nations Development Programme and the International Union of Conservation of Nature (IUCN).
In March, this year, the Ministry of Natural Resources and Tourism announced its plan to set aside 40 per cent of the total area of the Loliondo Game Controlled Area as a wildlife corridor, which would prohibit community residence or livelihood activities on the most important section of land for grazing and water access.
Press Briefing
White House Press Briefings are conducted most weekdays from the James S. Brady Press Briefing Room in the West Wing.
Waajiri wa Kenya watoa tahadhari kuhusu ubora wa wahitimu wa vyuo vikuu
Na Rajab Ramah, Nairobi
Mitaani kote Nairobi, ni rahisi kuona bango la chuo kikuu au maandishi ya kampasi ya chuo yakitangaza programu kadhaa na fursa za kusoma.

Wanafunzi kwenye hafla ya kuhitimu masomo katika chuo cha ufundi Technical University of Kenya huko Nairobi mwaka 2012. Shule hiyo mwanzo ilikuwa inaitwa Kenya Polytechnic University College na kupata hadhi ya chuo Kikuu mwezi Januari. [Na Rajab Ramah/Sabahi]
Ingawa hili linaweza kuwa dalili ya kuimarika kwa upatikanaji wa elimu nchini Kenya, baadhi ya waajiri na maafisa wa elimu wana wasiwasi kwamba kuenea kwa vyuo vikuu na kufanywa biashara kwa elimu ya juu kumeunda shule ambazo zinatoa wahitimu waliotayarishwa vibaya ambao hawakidhi mahitaji ya soko la ajira.
"Tunakosoa ubora wa elimu inayotolewa na vyuo vikuu vyetu," alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Shirikisho la Waajiri Kenya Jacqueline Mugo. "Wengi wa wahitimu tunaoajiri hawana ujuzi katika nyanja zao za masomo wa kuwasaidia waweze kushindana katika sehemu zao za kazi. Wanazo [shahada] nzuri sana ambazo hawawezi kuzitetea wakiwa kazini."
Mugo aliiambia Sabahi kwamba baadhi ya waendeshaji wa vyuo vikuu wanahatarisha ubora wa elimu kwa kuwakubali wanafunzi wasio na uwezo wa kuweza kukubalika katika chuo, na wanajali faida ya fedha tu wakati wanapanua na kutoa programu tofauti za elimu.
"Tulizoea kuona vyuo vikuu vikitoa utaalamu katika nyanja fulani, lakini sasa vyuo vikuu vyote vinatoa digirii kaitka kila, uwanja, ili waweze kupata fedha kutoka kwa wanafunzi wengi kadiri inavyowezekana. Kwa mwenendo kama huo, huwezi kuhakikisha mafunzo yenye ubora kwa wanafunzi," Mugo alisema, na kuongeza kwamba waajiri mara nyingi hulazimika kulipia ili kuwapa mafunzo wafanyakazi wao ili kuziba pengo la ujuzi.
Wednesday, May 22, 2013
U.S., Jordan blame Assad for Syria escalation at Amman conference
Diplomats pose after their Friends of Syria alliance meeting in Amman, May 22, 2013. (Reuters)
Al Arabiya with Agencies -
A conference gathering the Friends of Syria began on Wednesday in the Jordanian capital Amman to seek a political solution to the Syrian conflict, the main topic up for discussion is set to be the U.S.-Russian proposal for peace talks.
Delegates from Britain, Egypt, France, Germany, Italy, Jordan, Qatar, Saudi Arabia, Turkey, the United Arab Emirates and the United States attended the meeting.
The Jordanian Foreign Minister Nasser Judeh spoke during the opening session and said the aim of the talks is to develop plans for a political transition period to start in Syria.
During the opening session, U.S. Secretary of State John Kerry said forces loyal to Syrian President Bashar al-Assad escalated violence in the country.
The Jordanian foreign minister also added that the Syrian crisis left more than one hundred thousand as victims of war in the country until now.
Misumeno ya moto kutokomezwa
Na Hassan Hamad , OMKR
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, amewataka wananchi kushirikiana kuisaka misumeno ya moto popote ilipo ili iweze kutokomezwa kabisa katika visiwa vya Unguja na Pemba.
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad akiichoma moto misumeno ya moto 23 katika eneo la Kizimbani Pemba, ikiwa ni kampeni ya kutokomeza misumeno hiyo Zanzibar. (Picha, Salmin Said, OMKR).
Ameeleza hayo katika kampeni maalum ya kutokomeza misumeno ya moto ambapo misumeno 23 imechomwa moto mbele ya kiongozi huyo, baada ya kukamatwa na maofisa wa Idara ya misitu.
Amesema kila mtu ana wajibu wa kushirikiana na jamii katika kufichua misumeno iliyobakia, ili kuhakikisha kuwa haitumiki tena na kusababisha athari za kimazingira.
“Kila mtu ana wajibu wa kuwafichua watumiaji wa misumeno hii, lakini mashena na polisi jamii muna jukumu kubwa zaidi, na nina hakika mukiamua munaweza kuwabaini wote wenye misumeno ya moto”, alisema Maalim Seif.
Amesema iwapo misumeno hiyo haitodhibitiwa inaweza kuiathiri nchi kwa kiasi kikubwa kutokana na uwezo wake wa kukata miti kwa muda mfupi.
Uchomaji huo wa misumeno ya moto 23 umefanyika katika ofisi za Idara ya misitu iliyoko Kizimbani Kisiwani Pemba.
Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya kilimo na maliasili Affan Othman Maalim amesema misumeno ya moto ipatayo 270 bado inakisiwa kuwepo Zanzibar, na kwamba kampeni hiyo itasaidia kuitokomeza.
Kwa mujibu wa Affan, kisiwa cha Pemba kinaongoza kwa kuwa na misumeno mingi ya aina hiyo ipatayo 150, huku Unguja kukiwa na misumeno zaidi ya 120.
Amefahamisha kuwa takriban ekari 1000 za miti hupotea kila mwaka visiwani Zanzibar kutokana na kukatwa ovyo na kuongezeka kwa kasi hiyo kutokana na matumizi ya misumeno ya moto.
Naibu Waziri wa Kilimo na Maliasili Mtumwa Kheir Mbarak, amesema misumeno hiyo ambayo ni adui wa muda mrefu wa mazingira, inaweza kuiweza kuifanya nchi kuwa jangwa kwa muda mfupi na ni hatari pia kwa afya ya binadamu.
Maalim Seif yuko kisiwani Pemba kwa ziara ya kikazi ya siku mbili ambako anatembelea shughuli za kilimo kwa lengo la kuwahamasisha wakulima kuendeleza kilimo chenye tija kwa kutumia utaalamu wa kisasa na mbegu bora.
Katika Mkoa wa Kaskazini Pemba ambako alianza ziara yake alitembelea shamba la utafiti wa uzalishaji wa mpunga wa mbegu ya nerika liloko Gombeume mchangamdogo, skuli ya wakulima iliyoko Kiongweni Kambini, shamba la viazi vitamu Makangale na skuli ya wakulima juu ya nishati mbadala iliyoko Kinyasini.
Chanzo - zanzinews.com
Mpangilio wa Drone za Marekani zinawaua raia wasio na hatia

Shirika la kimataifa la kufuatilia migogoro (ICG) limetoa ripoti inayosema kuwa, ndege zisizo na rubani za Marekani zimekuwa zikiwaua kwa mabomu raia wa kawaida wasio na hatia nchini Pakistan kinyume na madai ya Washington kwamba ndege hizo zinatumiwa kulenga ngome za makundi ya kigaidi.
Shirika hilo lenye makao yake mjini Brussels, Ubelgiji limesema Marekani imeficha ukweli kuhusu mauaji ya raia nchini Pakistan na ameitaka White House kuweka wazi takwimu za raia wasio na hatia waliouawa kutokana na hujuma ya ndege hizo.
ICG imesema Marekani imekiuka sheria za kimataifa zinazolinda haki za binadamu na imeutaka Umoja wa Mataifa kuchunguza suala hilo. Marekani inatumia ndege zisizo na rubani katika nchi nyingi duniani ikiwa ni pamoja na Yemen na Somalia.
Machafuko Mtwara,Ofisi ya CCM yachomwa moto
MAPAMBANO kati ya Askari wa Jeshi la Polisi na Wananchi wa Mkoa wa Mtwara umefika katika hatua mbaya,kiasi cha mtu mmoja kudaiwa kujeruhiwa vibaya baada ya kurushiwa bomu wakati wa mashambulizi hayo katika eneo la Magomeni.


Mbali na kujeruhiwa kwa mtu huyo aliyekuwa katika maandamano ya kupinga Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini, Ofisi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) pia imechomwa moto.
Taarifa zilizonaswa na Fahari ya Kusini hivi punde zinadai kwamba wananchi wa Mkoa wa Mtwara wamefungiwa majumbani tangu asubuhi, huku Jeshi la Polisi likifanya msako wa nyumba hadi nyumba kwa lengo la kuwanasa watuhumiwa wanaodaiwa kuchochea maandamano hayo kwa njia ya vipeperushi.
Shuhuda wa wa tukio hilo ameitaarifu Fahari ya kusini kwamba waandamanaji hao wameapa kufa endepo serikali itaendelea na mipango yake ya kusafirisha gesi hiyo hadi Jijini Dar es Salaam.
"Hali hapa ni mbaya, tangu asubuhi wananchi wote wamefungiwa ndani ya majumba yao, hakuna anayeruhusiwa kutoka nje, Polisi wanapiga mabomu ya machozi kila mtaa huku wakiwasaka watuhumiwa waliosambaza vipeperushi na kuwatawanya wandamanaji waliozagaa katika mitaa mbalimbali, mpaka hivi sasa kuna mtu mmoja ameripotiwa kujeruhiwa vibaya katika mashambulizi ya raia na Asakari Polisi wanaotumia mabomu ya machozi na silaha zigine za moto"alisema shuhuda wa tukio hilo.

Hata hivyo imedaiwa kuwa hali hiyo imesababisha barabara zote kufungwa kiasi cha kuzuia mabasi yanayoingia na kutoka katika mji huo toka asubuhi, kuna baadhi ya mitaa matairi yamechomwa moto barabarani, magari ya FFU yametanda kila kona za mji, huku taarifa zidi ikifafanua kwamba hakuna mawasiliano, milio ya mabomu inasikika kila kona na hali ya utulivu sio ya kuridhisha, Askari wa zima moto wamesambaa kuzima moto na kuna baadhi ya nyumba maeneno ya Shangani zimechoma moto.
Nyumba ya mwandishi wa Habari wa TBC kassim Mikongoro inasemekana Imechomwa moto mchana huu. Hali ni tete Askari wawili na raia mmoja wanasadikika kuuawa.
Breaking News: Makinda ahairisha Bunge.
Spika wa Bunge Anna Makinda ameahirisha Kikao cha Bunge mpaka kesho serikali itakapotoa taarifa kamili kuhusiana na vurugu zinazoendelea huko Mtwara.
Chanzo - lindiyetu.blogspot.com
Zitto: wabunge wa Tabora wameshindwa kuwaletea barabara
Pamoja na Tabora kukosa barabara za kiwango cha Lami bado wabunge wake waliunga mkono bajeti wizara ya miundo mbinu kwa asilimia mia moja -zitto.
Kenyatta, Ruto named in Kenya TRJC report
Kenya’s President Uhuru Kenyatta and his deputy have been named in connection with post-election violence in a long-awaited report investigating human rights abuses in the country.

About 1,500 people were killed in the aftermath of disputed polls in 2007
The report gave no recommendation for action to be taken against Mr Kenyatta and Vice-President William Ruto. The report’s chairman told the BBC this was because they already face charges at the International Criminal Court.
Mr Kenyatta and Mr Ruto deny such allegations.
The Truth Reconciliation and Justice Commission (TRJC) was set up following deadly post-election clashes five years ago.
After those elections some 1,500 people were killed and more than 600,000 forced to flee their homes.
Its mandate was to investigate and recommend appropriate action on human rights abuses committed between Kenyan independence in December 1963 and the end of February 2008 – including politically motivated violence, assassinations, corruption and land disputes.
Bajeti Nishati kupoza kiu ya Wanamtwara?
Dodoma/Mtwara. Wakati mjadala mkali ukitarajiwa kuibuka bungeni leo wakati Serikali itakapokuwa ikiwasilisha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini, joto limezidi kupanda mkoani Mtwara ikielezwa kuwa wananchi wamehamasishana kwa mara nyingine kuacha shughuli zote ili kusikiliza kama hotuba hiyo italinda masilahi yao.

Profesa Sospeter Muhongo
Mjini Mtwara vipeperushi vinavyopingana vilisambazwa kuhamasishana ‘kuacha shughuli zao zote na kubaki nyumbani ili kufuatilia matangazo ya televisheni wakati Profesa Muhongo atakapotangaza bajeti hiyo, huku vingine vikipinga.
Ahadi za matumaini
Licha ya kampeni hizo za watu wa Mtwara, Serikali nayo imeweka matangazo katika vyombo vya habari likiwemo gazeti hili ikieleza namna mikoa ya Mtwara na Lindi itakavyonufaika na utafutaji na uendelezaji wa Gesi Asilia.
Tangazo lililotolewa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania limeainisha faida za gesi hiyo kwa Mkoa wa Mtwara ukiwamo umeme utakaotokana na gesi asilia. Pia imeelezwa jinsi mafunzo kwa vijana juu ya matatizo ya gesi asilia yaliyodhaminiwa na Wizara ya Nishati na Madini na kampuni mbalimbali kuanzia mwaka 2010.
Kilimanjaro 4. Inayotegemewa kuwasili Mwisho wa Mwenzi
Hii ndio boti mpya ya Kilimanjaro 4. Inategemewa kufika hapa mwishoni wa mwezi huu wa tano au mwanzoni mwa mwezi wa sita.
Inauwezo wa kubeba abiria 700 na kutumia muda wa dakika 70 kwa safari moja ya kwenda Zanzibar au Dar Es Salaam.

Ni boti mpya kabisa katika muendelezo wa boti za Kilimanjaro.
Boti hii itakidhi kiu ya wasafiri wa eneo hili kwa kuwa itakuwa na sifa zote, ambazo ni Usalama, Kasi zaidi, na unadhifu. Chanzo - ZanziNews
Katibu mkuu wa Umoja wa mataifa UN Ban Ki Moon ahimiza operesheni za kijeshi kuharakishwa mashariki ya DRC.
Na Martha Saranga Amini
Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa UN, Ban Ki Moon amesisitiza kuharakishwa kwa operesheni ya kijeshi ya vikosi maalumu vya Umoja wa mataifa kukabiliana na uasi mashariki mwa jamuhuri ya demokrasia ya Congo,uasi ambao umeanza kushuhudiwa juma hili ukukithiri wakati huu akiwasili mjini Kinshasa tayari kuzuru eneo la mashariki.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon asisitiza operesheni dhidi ya uasi kuanza haraka mashariki ya jamuhuri ya demokrasia ya Congo. /AFP
Katibu mkuu Ban amesema kuwa kulingana na hali iliyojitokeza juma hili kwa waasi kushambulia makazi ya watu na wanajeshi wa serikali, hakuna budi zaidi ya kuharakisha kusambazwa kwa wanajeshi wa UN kukabiliana na wapiganaji hao kikamilifu.
Kwa upande wa serikali ya DRC, imesema kuwa inashangazwa na waasi wa M23 kutaka kung'ang'aniza kukutana na katibu mkuu licha ya yeye mwenyewe kuwataka kwanza kuweka silaha chini ndipo wafanye mazungumzo.
Nao wabunge wa bunge la kitaifa wamekosoa kauli ya baadhi ya wabunge wa upinzani ambao wanataka kukutana peke yao na katibu mkuu na kuongeza kuwa wanashangazwa na hatua hiyo kwakuwa sasa walipaswa kuonesha umoja.
Katibu mkuu Ban Ki Moon anaanza ziara rasmi nchini DRC ambapo atakuwa na mazungumzo na rais Joseph Kabila mjini Kinshasa kabla ya kuelekea mashariki mwa nchi hiyo kushuhudia hali ilivyo.
Subscribe to:
Posts (Atom)
