Wadau wa facebook

Maelezo

Kwa matukio na matangazo wasiliana nasi Simu no' {301}728-3977. Email:swahilivilla@gmail.com

Friday, September 3, 2010

WASWAHILI HUSEMA ULIMI HAUNA MFUPA!

Msemo huo husemwa sana pale mtu anapokuwa amekosea kutamka neno au kutamka neno ambalo hakulimaanisha kwa wakati ule.

Msemo huu umemkuta mbunge wa Handeni Tanga Dk.Abdallah Kigoda baada ya bila kujifahamu alijikuta akimnadi aliyekuwa Rais wa awamu ya tatu Bw. Benjamin William Mkapa kwa kusema (Mkapa Oyeeee….!!!) badala ya mgombea urais wa sasa kupitia chama tawala CCM Rais Jakaya Mrisho Kikwete.

Dk.Kigoda alikutwa na mahasibu hayo wakati wa ufunguzi wa kampeni za mgombea ubunge kupitia chama hicho jimbo la Kilindi Bi. Beatrice Shelukindo zilizofanyika katika kijiji cha Kwediboma

No comments:

Post a Comment