
Rais Rene Preval.
Katika uchaguzi huo wa awamu ya kwanza wasimamizi wa kimataifa walisema kuwa matokeo hayo yalikuwa na udanganyifu.
Awamu ya pili ya uchaguzi huo ilipaswa kufanyika wiki mbili zilizopita lakini uliahirishwa kufuatia vurugu zilizozuka nchini humo.
Tume hiyo imefafanua kuwa matokeo ya mwisho ya awamu ya pili ya uchaguzi huo yatatangazwa aprili 16, 2011.
Taarifa ya kutangazwa kwa matokeo hayo imekuja wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani bibi Hillary Clinton akitarajiwa kuwasili Haiti hapo kesho kwa mazungumzo na rais Rene Preval kuhusu mgogoro wa uchaguzi, ukarabati baada ya tetemeko la ardhi na kulipuka kwa ugonjwa wa kipindupindu.

No comments:
Post a Comment