"May be hoping for a change is a dream, may be life aint as bad as it seems, but if dreaming is the best i can do, then i'll be dreaming my whole life through" Tanya Stephens Maneno haya ya mwanadada huyu niliyaeleza vema kwenye kipengele hiki hapa. Na kubwa hapa ni kuhusu NGUVU YA KUAMINI NA KUENDELEA KUOTA KATIKA KILE UAMINICHO.
Lakini pia nakumbuka kuwa "kichwa hiki cha post" nilishakitumia katika post hii niliyozungumzia ndoto za Dadangu Lady Jay Dee na zangu pia na kama nilivyosema katika post hiyo, ilikuwa ni MAALUM KWA NDUGU ZANGU WALIOKATA TAMAA YA KUTIMIA KWA NDOTO ZAO.
Katika maisha nimejifunza mengi sana. Na pia nimejifunza kujaribu kurejesha fikra za muunganisho wa matukio ili kuweza kuthamini pale ulipo. Na hili ni tatizo kwa wengi. Watu wengi wameshindwa kuoanisha kilichorokea na kinachotokea sasa na matokeo yake wanashindwa kuwa na FADHILA kwa wale waliowawezesha kufanikiwa walivyo (iwe ni kwa heri ama kwa shari).
Niliwahi kueleza HAPA mkasa wa mfanyakazi mwenzangu ambaye nipokutana naye wiki hiyo alinieleza kuwa ANAMSHUKURU MUNGU KUWA HAKUPATA NAFASI YA PROMOTION ALIYOKUWA ANAITAFUTA KWANI KULE ALIKOTAKA KUHAMIA NDIKO WALIKOPUNGUZA WENGI NA WALIPUNGUZA WASIO NA UZOEFU NA KAMA ANGEHAMIA ANGEKUWA HANA UZOEFU WOWOTE.
Habari hiyo ilinivutia saana nikaona nimualike kwenye Club yetu chuoni aweze kuzungumza na kuwahamasisha wanasayansi watarajiwa, na mwezi march mwaka 2009, alikuja chuoni na kuzungumza nasi. WATU WAKAPENDA NA KUJIFUNZA..Bofya hapa kwa kuendelea kusoma Zaidi. ChangamotoYetu
Dr Thomas nami March 4, 2009.
Baada ya mazungumzo hayo, nilitamani saana kushirikisha wenzangu katika alichozungumza, lakini kwa bahati mbaya SIKUWEZA. Ni kwa kuwa mengi ya aliyozungumza sikuyakumbuka kwa usahihi hivyo nikaona NI VEMA KUMTAFUTA, KISHA NIMREKODI NA KUWEZA KUSHIRIKIANA NA WAPENDWA HAPA. Nilijaribu kiasi (unakumbuka HII POST? l
Baada ya mazungumzo hayo, nilitamani saana kushirikisha wenzangu katika alichozungumza, lakini kwa bahati mbaya SIKUWEZA. Ni kwa kuwa mengi ya aliyozungumza sikuyakumbuka kwa usahihi hivyo nikaona NI VEMA KUMTAFUTA, KISHA NIMREKODI NA KUWEZA KUSHIRIKIANA NA WAPENDWA HAPA. Nilijaribu kiasi (unakumbuka HII POST? l
Sikiliza sehemu HII fupi kati ya saa moja la mahojiano yangu na Dr Donald. Nimeweka sehemu ya HISTORIA, HARAKATI ZAKE KUJIUNGA NA NASA, ALIVYOKATA TAMAA BAADA YA KUONA AMEKOSA NAFASI HIYO, HISIA ZAKE SIKU ALIPOPATA na mwisho WITO WAKE KWETU... FURAHIA UKIJIFUNZA










Abou Shatry Mzee wa Swahili Villa blog akiwa kapandwa na mzuka kwenye show ya King Kiki. Picha kwa hisani ya 








