
Zimepokelewa hadithi nyingi zinazotujulisha kuwa Siku ya Ijumaa ni siku tukufu kupita siku zote.
Mtume (SAW) amesema;
"Siku tukufu kupita zote ni Siku ya Ijumaa, hiyo ndiyo siku aliyoumbwa Adam (AS) na siku hiyo aliingizwa Peponi, na siku hiyo ndiyo aliyotolewa humo, na Kiama hakitosimama katika siku nyingine isipokuwa siku (hii) ya Ijumaa".
Muslim: Dua ndani yake
Zimepokelewa hadithi nyingi pia kuwa katika Siku ya Ijumaa upo wakati maalum ambao dua ndani yake inakubaliwa.
Kutoka kwa Abu Saeed na Abu Huraira (Radhiyallahu anhum) wamesema;
"Mtume (SAW) amesema;
"Siku ya Ijumaa ina masaa kumi na mawili. Ndani yake mna saa maalum ambayo mja yeyote Muislam ikimkuta saa hiyo akiwa anaomba dua ya kheri basi inakubaliwa - na itafuteni zaidi (saa hiyo) katika nyakati za mwisho wa mchana".
Annasai - Abu Daud - Al Hakim - na akasema kuwa hadithi hii ni sahihi kufuatana na masharti yaliyowekwa na Imam Muslim
Kukithiri kumsalia Mtume (SAW) ndani yake
Kutoka kwa Aus bin Aus (RA) amesema kuwa Mtume (SAW) amesema;
"Siku tukufu kupita zote ni Siku ya Ijumaa, ndani yake ameumbwa Adam na siku hiyo ndiyo siku litakapopulizwa (baragumu) na siku hiyo ndiyo watu wote watakapokufa. Kwa hivyo nisalieni sana siku hiyo (ya Ijumaa) kwani ninafikishiwa Sala zenu".
Imeotelwa na maimam wote watano (wa hadithi) isipokuwa Attirmidhiy
Endelea kusoma http://mawaidha.info/salayaijumaa.htm

No comments:
Post a Comment