Wadau wa facebook

Maelezo

Kwa matukio na matangazo wasiliana nasi Simu no' {301}728-3977. Email:swahilivilla@gmail.com

Saturday, April 14, 2012

Balozi Seif Ali Idd afanya mazungumzo na Balozi Mpya wa Jamuhuri ya Watu wa China Bw. Lu Youqing

Na Othman Khamis Ame Zanzibar

Zanzibar inaendelea kufaidika na sekta ya Michezo kufuatia kukamilika kwa ujenzi wa Uwanja wa Michezo wa Amani miaka michache iliyopita uliojengwa na Serikali ya Jamuhuri ya watu wa china.


Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alieleza hayo wakati wa mazungumzo yake na Balozi Mpya wa China Nchini

Tanzania Bwana Lu Youqing aliyefika Zanzibar kujitambulisha rasmi. Mazungumzo ya Viongozi hao wawili yalifanyika kwenye Ofisi ya Balozi Seif iliyoko katika Jengo la Baraza la Wawakilishi Mbweni nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Balozi Seif alisema Uwanja wa amani umezidi kuwa na hadhi zaidi ya kuchezewa kwa mechi za kimataifa na kukifanya kuwa miongoni mwa Viwanja muhimu ndani ya ukanda wa Afrika Mashariki.

Aliipongeza Jamuhuri ya watu wa china kwa Makampuni yake kuendelea kutoa huduma hapa Nchini na kuelezea matumaini yake ya Zanzibar kuwa na kiwanja chengine cha Kimataifa hapo baadaye.

Alieleza kuwa uwanja huo uliopewa jina la Kiongozi wa China Mao Tse tung unatarajiwa kujengwa upya ili kukidhi mahitaji ya wana michezo nchini.

Balozi Seif alisema uwanja huo utakapomalizika unatarajiwa kuwa na uwezo wa kutoa huduma nying za michezo pamoja na shughuli za Kitaifa ikiwemo ile maarufu ya gharide katika sherehe mbali mbali.

No comments:

Post a Comment