Wadau wa facebook

Maelezo

Kwa matukio na matangazo wasiliana nasi Simu no' {301}728-3977. Email:swahilivilla@gmail.com

Friday, April 27, 2012

Charles Taylor atiwa hatiani

Charles Taylor akisikiliza maelezo ya kesi yake.
Aliyekuwa rais wa Liberia Charles Taylor amepatikana na hatia ya kutenda uhalifu wa kivita kwa kuyapa makundi ya waasi wa Sierra Leon silaha ili kujipatia almas za damu. Hukumu yake inatarajiwa kutolewa Mei 30 mwaka huu.

Hakimu aliyeongoza kesi hiyo Richard Lussick alimuambia Taylor kuwa ana hatia ya kusaidia katika uhalifu wote uliotendwa nchini Sierra Leon: "Mshatikiwa kwa matendo yake ana hatia yeye binafsi ya kusaidia kupanga, kutayarisha na kutenda uhalifu unaotajwa katika ibara za 3 na 4 za sheria kama ilivodaiwa katika mashtaka."

Hakimu Lussick aliongeza kuwa matendo ya Taylor alikuwa na ushawishi mkubwa katika uhalifu uliotendwa na alikuwa na dhamira ya kuchukua hatua ili kusaidia na kuunga mkono uhalifu. Baada ya kutolewa hukumu, Taylor atatumikia adhabu ya kifungo katika jela nchini Uingereza.
Taylor kama mmoja wa makatili wakubwa barani Afrika

Kama kiongozi wa waasi, mbabe wa kivita na baadae mkuu wa nchi, Taylor hakuwatesa tu raia wake nchini Liberia, bali pia aliwaunga mkono waasi wa Sierra Leon waliyofanya ukatili wa kutisha dhidi ya wananchi ikiwa ni pamoja na kuwakata mikono na vidole.

Katika kuunga mkono waasi wa Sierra Leon, lengo la Taylor lilikuwa kupata udhibiti wa migodi ya madini ya almas ya nchi hiyo jirani na Liberia na kuuza kile kilichokuja kuitwa almas za damu ili kuendesha vita vyake nchini Liberia vilivyochukua muda wa miaka 10 na kusababisha vifo vya watu laki moja na elfu 20.

No comments:

Post a Comment