Na Faki Mjaka-Maelezo Zanzibar
Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kushirikiana na Jamhuri ya Kiislam ya Iran zimeunda timu ya watu wanne ambao watasimamia upatikanaji wa Mtambo wa kuchapishia magazeti ya Serikali ya Zanzibar ili kuyafanya magazeti hayo kuchapishwa Zanzibar badala ya Dar es Salaam.
Timu hiyo inajumuisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari Utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar Dk.Ali Mwinyikai na Mkurugenzi wa Idara ya Makumbusho Dk.Amina ambao watasaidiana na maofisa wawili wa Iran katika kuhakikisha upatikani wa Mtambo huo.
Hatua hiyo imekuja kufuatia ziara ambayo imefanywa na Balozi wa Iran nchini Tanzania Morahhed Ahom wakati alipomtembelea Waziri wa Habari utamaduni Utalii na Michezo Zanzibar Said Ali Mbarouk ofisini kwake Kikwajuni mjini Zanzibar kuzungumzia masuala mbalimbali ya nchi hizo.
Morahhed amesema kwa vile Zanzibar na Iran ni nchi ambazo zina uhusinano wa muda mrefu hivyo kuna kila sababu ya Iran kuisaidia Zanzibar katika mambo ambayo yamo ndani ya uwezo wao.
Miongoni mwa mambo ambayo Iran imeahidi kuyafanyia kazi ni pamoja na kusaidia ukarabati wa magofu ya Zanzibar ambayo yamekuwa kivutio kikubwa kwa watalii kutoka pande zote za dunia.

Sudanese President Omar Bashir
Party: Fifteen-year-old girls pose for a group picture at the Franz Mayer museum before a mass 'Quinceanera' birthday celebration in Mexico City on Saturday, April 28, 2012

Kukataa huko kwa wanajeshi kumezua ukungu wa shaka katika makubaliano ya mwezi uliopita ya kutatua mkwamo wa kisiasa nchini humo.
Finance minister Maria Kiwanuka


