Wadau wa facebook

Maelezo

Kwa matukio na matangazo wasiliana nasi Simu no' {301}728-3977. Email:swahilivilla@gmail.com

Tuesday, July 31, 2012

Benki ya CBA kuisaidia Zanzibar kununua Meli mpya

Na Mohammed Mhina, Zanzibar

Nae balozi Seif Idd ameshukuru msaada huo kutoka CBA na ametoa wito kwa wadau mbalimbali na serikali kuitembelea benki hiyo ili kuona ni jinsi gani taifa linaweza kufaidika hasa kwenye kuisaidi serikali kuboresha usafiri majini

Afisa Mtendaji mkuu wa benki ya CBA, Bw Yohane Kaduma akimkabithi mfano wa hundi yenye thamani ya Tsh Millioni 5 kwa makamu wa pili wa Raisi wa Zanzibar Balozi Seif Idd.

Wakati Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ikiwa kwenye mchakato wa kutafuta fedha za kununua meli mpya, Benki ya Biashara ya Afrika (CBA), imesema iko tayari kuikopesha SMZ fedha za kununulia Meli hiyo.

Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki hiyo Bw. Yohane Kaduma, amesema benki yake iko tayari kuipitia SMZ mkopo wa kununulia Meli hiyo endapo watakubaliana na kushirikishwa kwenye mchakato huo.

Bw. Kaduma alikuwa akizungumza na Waandishi wa Habari mjini Zannzibar mara baada ya kukabidhi msaada wa shilingi milioni 5, kwa Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibat Balozi Seif Ali Iddi ili kusaiidia ghala za matibabu kwa majeruhi na ubani kwa wafiwa wa ajali ya Meli ya Skagit.

Bw. Kaduma amesema kuwa endapo Benk yake itaombwa kutoa mkopo huo inaweza kufanya hivyo ili mradi tu kukaa meza moja na Serikali na kukubaliana aina ya mkopo pamoja na mambo mengine.

Awali akipokea msaada huo, Makam wa pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi, amesema kuwa pamoja na kusimamishwa kwa baadhi ya meli za watu binafsi kuchukua abiria, SMZ pia imeagiza meli zake kufanyiwa uchunguzi kama zinafaa kuchukua abiria.

Balozi Seif amesema kuwa ameziagiza Mamlaka ya usafiri majini Zanzibar na Sumatra, kuzifanyia uchunguzi meli hizo za SMZ ikiwemo MV Maendeleo ambayo imerejea siku za karibuni ikitokea Mombasa nchini Kenya ambako ilikuwa katika matengenezo makubwa.

Amesema Serikali haiwezi kukaa kimya huku ikiona kuwa wananchi wake wanapatwa na majanga ya mara kwa mara kutokana na kusafiri kwa meli zisizo na uhakika.

Sikiliza kwa makini Hotuba ya Mwalimu Nyerere, Mkutano Mkuu wa CCM Dodoma - 1995

Dk Shein Afutarisha Pemba

Na Rajab Mkasaba, Ikulu

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Ali Mohamed Shein aliungana na wananchi wa Mkoa wa Kaskazini Pemba katika futari maalum aliyowaandalia wananchi hao.

Hafla hiyo ilifanyika huko katika viwanja vya Ikulu ndogo ya Wete na kuhudhuriwa na wananchi hao pamoja na viongozi mbali mbali wa dini, Serikali na vyama vya siasa.

Miongoni mwa viongozi hao ni pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba Mhe. Dadi Faki Dadi, Waziri wa Nchi Afisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk.Mwinyihaji Makame, Mufti Mkuu wa Zanzibar Sheikh Saleh Omar Kabih.

Akitoa neno la shukurani kwa mahudhurio yao makubwa wananchi hao kwa niaba ya Alhaj Dk. Shein, Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Pemba alieleza kuwa Dk. Shein amefarajika kwa ushiriki wa wananchi hao katika futari hiyo maalum aliyowaandalia.

Nao wananchi hao walieleza kufarajika kwao na muwaliko huo wa Rais na kueleza kuwa hatua yake hiyo inaonesha wazi mapenzi, busara, hekima na jinsi anavyowajali wananchi wake pamoja na maamrisho ya MwenyeziMungu na Mtume wake Mohammad S.A.W.

Wananachi hao walimuombea dua kwa MwenyeziMungu na kumuombea aendelee kongoza nchi kwa salama, amani, utulivu na uvumilivu mkubwa sanjari na kuendelea kuongoza nchi kwa kupata maendeleo makubwa.

Wakati huo huo pia. Mama Mwanamwema Shein nae alishiriki katika futari hiyo akiungana na akina mama wenzake kutoka sehemu mbali mbali katika Mkoa huo pamoja na viongozi wa dini, serikali na vyama vya siasa na wananci kwa ujumla.

Msaidizi wa Mitt Rommney Mgombea Uraisi wa Marekani (R) Atukana Waandishi wa Habari!

Na Tanga Pia Wapendekeza Katiba Mpya ifute Muungano

Burhani Yakub, Tanga

MUUNDO wa sasa wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,unapaswa kufanyiwa marekebisho kupitia Katiba Mpya, ili kupunguza manung’uniko na hatimaye mwafaka kuhusu Muungano.

Hayo yalisemwa juzi na wananchi wa Jiji la Tanga, walipokuwa wakitoa maoni yao kwa Tume ya Kukusanya Maoni ya Wananchi kuhusu Mabadiliko ya Katiba Mpya.

Wananchi hao, wamedai kuwa muundo wa sasa wa Muungano hauna tofauti na kuwaunganisha tembo na sungura, jambo ambalo haliletin usawa.

Akitoa mapendekezo yake, Jonathan Bahweje alisema kimsingi muundo wa sasa wa chombo hichon haufai kwa sababu hakuna fursa sawa kati ya Zanzibar na Tanzania bara.

“Muungano wa sasa ni kama tembo na sungura, unawaweka pamoja halafu unasema umewaunganisha na wako sawa, wakati kwa uhalisia, haiwezekani,” alisema Bahweja.

Mwananchi huyo alipendekeza Katiba Mpya, ivunje muungano ili usiwepo
hatimaye Tanzania bara na Zanzibar, kila moja ijitegemee na kwamba hakuna sababu ya kuogopa kuuvunja chombo hicho.

“Mimi napendekeza Muungano uvunjwe ili kila nchi iwe na Serikali yake, kwa sababu manung’uniko ni mengi na yanayotokana na jinsi muundo wa sasa usivyokubalika,”alisema Bahweja.

Alisema kama kuna ugumu wa kuvunja Muungano, basi ni vema kukawa na Serikali tatu, ili kila nchi iweze kuwa na uhuru wa kuendesha mambo yake wakati kuna Serikali ya Muungano itakayosimamiwa masuala yanayohusu Muungano tu.

Two suspected Ebola deaths reported in Uganda

KAMPALA (Reuters) – Two more people, including a child, are suspected to have died of the Ebola virus while 11 more have been put in isolation in western Uganda where the deadly haemorrhagic fever was first confirmed last Friday, health workers said on Tuesday.

So far 14 people have died of the disease and Ugandan officials fear a repeat of an outbreak in 2000, the most devastating to date, when 425 people were infected, more than half of whom died.

Dan Kyamanywa, health officer for Kibaale district where the outbreak had started, told Reuters by telephone that villagers had called medical officials on Tuesday to report that two more people had died, including a 5-year old boy.

Kyamanywa said the latest deaths also occurred in Kibaale, about 170 km (100 miles) west of the capital, and near the Democratic Republic of Congo where the virus first emerged in 1976, taking its name from the Ebola River.

“We got calls this morning about these two deaths which occurred in two different villages yesterday (Monday) evening,” he said. “The team that we sent says the initial clinical signs that the patients exhibited are typical of Ebola … also since yesterday, we have admitted 11 more suspected Ebola patients who are now in isolation.”

On Monday Uganda’s President Yoweri Museveni advised people to avoid shaking hands, casual sex and do-it-yourself burials to reduce the chance of contracting Ebola virus.

Dkt Migiro akutana na Jaji Warioba leo

Aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Dkt.Asha-Rose Migiro (kushoto) akimsikiliza Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko yaKatiba Jaji Mstaafu Joseph Warioba wakati Dkt. Migiro alipotembelea ofisi zaTume jijini Dar es Salaam leo (Julai 31, 2012). (Picha na Ismail Ngayonga).

Security in focus as Clinton heads to Africa

U.S. Secretary of State Hillary Clinton departs this week on a trip that will take her both to Africa’s newest nation, South Sudan, and on a visit to the continent’s elder statesman, 94-year-old anti-apartheid icon Nelson Mandela.

US Secretary of State Hillary Clinton

While Clinton’s public focus will be on Africa’s democratic achievements and economic potential, the trip also underscores U.S. security ties in the face of an array of growing threats –from Islamist extremists to narcotics cartels.

“The security threats are becoming much more visible and in some ways dangerous than they were before,” said Jennifer Cooke, the head of the Africa program at the Center for Strategic and International Studies in Washington.

“There are big global issues on the table, and the U.S. does not have the kind of finances available to mount splashy new economic initiatives in Africa.”

Clinton’s trip — potentially her last as America’s top diplomat — begins on Tuesday in Senegal, and continues on to South Sudan, where she will be the most senior U.S. official to visit since the country declared independence in July 2011.

Further stops include Uganda, Kenya, Malawi and South Africa, the State Department said.

Clinton is expected to highlight U.S. programs on development, education and HIV/AIDS — long the backbone of U.S. engagement with Africa — as well as U.S. economic interest in a continent whose rich resources and enviable growth rates have drawn rival suitors including China and India.

She will also likely emphasize projects for women and girls, one of her central themes in a job she says she will leave in January even if President Barack Obama is elected to a second term.

But Clinton’s visit is also part of a U.S. push to broaden security partnerships with key countries such as Uganda and Kenya — ties that are growing fast despite sometimes serious U.S. concerns over democratic governance.

Wanajeshi wa serikali iliyoangushwa Mali wateswa

Malian junta soldiers patrol a road in Kati, outside Mali's capital Bamako, April 1, 2012. Mali's junta leader promised to reinstate the constitution from Sunday, hours before a deadline set by West African neighbours to start handing over power, and as rebels encircled the ancient trading post of Timbuktu. Amadou Sanogo, who led a military coup on March 22, also pledged to re-establish all state institutions before organising a transfer of power back to civilians through democratic elections. REUTERS/Luc Gnago (MALI - Tags: MILITARY POLITICS)
Shirika la Kimataifa la kutetea haki za binaadamu Amnesty International limesema wanajeshi watiifu kwa serikali iliyoangushwa Mali wameteswa na haki zao nyingine kukiukwa mikononi mwa jeshi lililofanya mapinduzi.

Katika ripoti iliyotolewa leo nchini Ufaransa, shirika hilo limesema wanajeshi hao aidha walitoweka au kuuawa mbali na kuteswa wakati walipowekwa kizuizini baada ya kushiriki katika jaribio jingine la tarehe 30 Aprili kutaka kulipindua jeshi lililokuwa limeiondoa serikali ya kiraia mnamo Machi 22.

Ripoti hiyo ya Amnesty International, ambayo inakuja siku kumi baada ya ujumbe wa kutathmini hali halisi nchini Mali mnamo mwezi Julai, ina matukio ya visa vya ukiukaji wa haki za binaadamu vilivyofanywa na wanajeshi watiifu kwa uongozi wa kijeshi dhidi ya wanajeshi na polisi waliohusishwa na mapinduzi ya pili ya kuliondoa jeshi.

Shirika hilo limewataka maafisa wa Mali kusitisha vitendo vya ukiukaji wa haki za binaadamu na kuanzisha uchunguzi kuhusu visa kadhaa vya kutoweka kwa watu, mauaji ya kiholela na mateso.

Serikali ya Umoja wa Kitaifa

Hayo yanajiri wakati rais Traore akikabiliwa na muda wa mwisho leo uliowekwa na Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi ECOWAS kuunda serikali ya umoja wa kitaifa, ambayo inatarajiwa kuweza kukabiliana na uvamizi wa upande wa kaskazini uliofanywa na wanamgambo wa kiislamu wenye misimamo mikali.

Commercial Bank of Africa set to support Zanzibar new ferry deal

By Teonas Aswile

As the Revolutionary government of Zanzibar is in the process of ‘boosting the pockets’ to buy a new ferry the Commercial Bank of Africa (CBA) has said it is ready to support the government on the deal.


Chief Executive Officer of Commercial Bank of Africa (CBA), Yohane Kaduma (L) handing a cheque worth Tsh 5 Mil to the Second Vice President of Zanzibar, Ambassador Seif Ali Iddi for MV Skagit victims.

Speaking to journalists few minutes after handing Tsh 5 Mil bank support to MV Skagit victims to Second Vice President’s office of Zanzibar, Chief Executive Officer of CBA, Yohane Kaduma said CBA is ready to grant loan to the government of Zanzibar if it is involved in the process.

Apart from granting a loan, Kaduma said the bank wishes to see the citizens of Zanzibar travel in safe environment from any marine troubles.

Earlier during the reception of the victims support, Second Vice President of Zanzibar, Ambassador Seif Ali Iddi said more investigation is conducted on the private ferries which have been stopped to operate.

“The government has ordered the Maritime authority in Zanzibar and SUMATRA to investigate even our ship, MV Maendeleo which was in maintenance in Mombasa-Kenya.”

Na Gazeti la mwananchi: Koti la Muungano lawabana vijana, vikongwe Zanzibar

Masoud Sanani

VIJANA na wananchi wenye umri mkubwa (vikongwe) wa Mkoa wa Kusini Pemba wengi wao wameonyesha kuwa hawataki Muungano uliopo sasa nchini Tanzania.

Vijana na wazee wachoshwa na koti la muungano Pemba.

Wakitoa maoni yao mbele ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba inayochukua maoni kutoka wananchi wa Mkoa wa Kusini Pemba, vijana wengi na vikongwe wamekuwa wakieleza kuwa hawataki Muungano.

Hata wale ambao wanataka mfumo mwingine wa Muungano, wanasema huu wa sasa haufai, bali wanapendekeza kuwe na Muungano wanaouita wa mkataba.

Wale ambao waliulizwa na wajumbe wa Tume ya Katiba Muungano wa mkataba una maana gani, wengi walieleza kuwa baada ya Zanzibar kuwa na Serikali yake yenye mamlaka kamili na Tanganyika nayo kuwa na Serikali yake, Serikali hizo mbili zitatoa wajumbe watakaounda Serikali ya Muungano ambayo wanaeleza kuwa ni ndogo.

Vijana na vikongwe ambao hawataki Muungano wanasema kwamba hauna faida yoyote kwa Zanzibar na umekuwa ukiwadhulumu haki zao, na unapendelea zaidi upande wa Tanzania Bara.

Mambo makubwa ambayo yamekuwa yakilalamikiwa na wananchi walio wengi ni ajira katika Jeshi na Polisi na mgawanyo wa mabalozi wa Tanzania nje ya nchi na hata wafanyakazi wa balozi hizo kuwa zina Wazanzibari wachache mno.

Pia wanaeleza kuwa wakuu wa vyombo vya ulinzi, Jeshi na Polisi hawajawahi kutoka Zanzibar, pia Gavana wa Benki Kuu na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Wananchi hao pia walieleza kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tananzania kila wakati anatoka Tanzania Bara na mwananchi mmoja akadai kuwa hata aliyekuwa Rais wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi hakuwa Mzanzibari halisi.

White House wants Romney to explain Israel remarks

Republican presidential hopeful Mitt Romney the midst of a three-nation tour, gave a speech Sunday in Jerusalem where he hailed the city as “the capital of Israel,” in apparent support of a position held by the Jewish state but never accepted by the global community. (Reuters) Republican presidential hopeful Mitt Romney the midst of a three-nation tour, gave a speech Sunday in Jerusalem where he hailed the city as “the capital of Israel,” in apparent support of a position held by the Jewish state but never accepted by the global community. (Reuters)

By AFP, WASHINGTON

The White House called Monday on Republican presidential hopeful Mitt Romney to explain recent remarks including his apparent endorsement of Jerusalem as Israel’s capital, a position that counters U.S. policy.

Romney, in the midst of a three-nation tour, gave a speech Sunday in Jerusalem where he hailed the city as “the capital of Israel,” in apparent support of a position held by the Jewish state but never accepted by the global community.

The comment was swiftly rejected by Palestinian negotiator Saeb Erakat as “unacceptable” and “harmful to American interests in our region.”

But after Romney made fresh controversial statements Monday to donors in Jerusalem including suggesting Israeli “culture” helped explain the country’s economic success -- a position Erakat denounced as “racist” -- President Barack Obama’s office urged Romney to clarify his comments.

Mtikisiko

WALIMU WAGOMA KILA KONA, WANAFUNZI NAO WACHACHAMAA, SERIKALI YAONYA, YATISHIA KUWAFUTIA MISHAHARA

Waandishi Wetu
NCHI imetikiswa. Mgomo wa walimu ulioanza jana katika sehemu mbalimbali nchini, umeathiri kwa kiasi kikubwa sekta ya elimu huku kukiwa na taarifa za matukio yasiyokuwa ya kawaida yaliyoambatana na mgomo huo usio na ukomo.

Katika sehemu mbalimbali nchini, walimu waliripotiwa kugoma kwa kutoingia madarasani na wengine walifika kazini na kusaini vitabu vya mahudhurio kisha kuondoka hali iliyosababisha wanafunzi kurandaranda ovyo katika sehemu za miji iliyo karibu na shule hizo.

Mjini Dodoma ,wabunge jana walimbana Naibu Spika, Job Ndugai wakitaka shughuli za Bunge zisitishwe ili kujadili mgomo wa walimu ambao umeanza rasmi jana nchi nzima, na kuziacha shule nyingi zikiwa na walimu wakuu na wakuu wa shule pekee.

Hata hivyo, Ndugai alisema Bunge lisingeweza kujadili suala hilo kwani tayari Serikali ilikuwa imelifikisha mahakamani baada ya kushindwa kuafikiana na walimu katika ngazi ya usuluhishi.Wakati hayo yakiendelea, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk Shukuru Kawambwa amesema Serikali itafuta mishahara kwa walimu walioitikia mwito Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wa kushiriki mgomo ambao alisema siyo halali.

Katika mkutano wake na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Dk Kawambwa pia aliwaonya walimu ambao alisema wamekuwa wakiwabughudhi wenzao ambao waliamua kwenda kazini.

Kwa upande wake, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo akiwa Mjini Morogoro aliwaagiza wakuu wa shule za msingi na sekondari mkoani humo kuandaa orodha ya majina ya walimu wasiofika kazini Julai 30 na waifikishe kwa maofisa elimu wa wilaya kabla ya saa 2:00 asubuhi ya Julai 31.

Waandishi wetu katika sehemu mbalimbali nchini pia waliripoti kwamba katika baadhi ya shule, wanafunzi waliruhusiwa kurejea nyumbani mapema kwa maelezo kwamba hakukuwa na masomo.


Hali hiyo ilizua kizaazaa kwani katika baadhi ya mikoa wanafunzi walicharuka na kuitisha maandamano hadi katika ofisi za maofisa elimu wa wilaya, wakitaka Serikali iingilie kati mgomo huo ili waendelee kusoma.

Kadhalika, baadhi ya viongozi na watendaji wa Serikali walinukuliwa wakitoa matamko ya kuwasihi au kuwaamuru walimu warejee madarasani, kauli ambazo hata hivyo, hazikubadili uamuzi wa walimu hao.

Wanafunzi waandamana

Maandamano ya wanafunzi yaliripotiwa katika Mji wa Tunduma, Mbeya ambako polisi walitumia mabomu ya machozi kuwadhibiti wanafunzi.

Wanafunzi wa shule mbalimbali za msingi katika Wilaya ya Mbozi mkoani humo waliandamana wakidai haki ya kufundishwa. Hata hivyo, maandamano hayo yaliingiliwa na vibaka ambao baadaye walivunja ofisi za Halmashauri ya Mji wa Tunduma na kuiba mali kadhaa kisha kuchoma nyaraka zilizokuwemo.

Tukio hilo lilitokea asubuhi wakati wanafunzi wa shule 14 za msingi zilizopo katika halmashauri ya Tunduma walipojikusanya na kufanya maandamano hadi nyumbani kwa diwani na baada ya kumkosa walielekea kituo cha polisi na baadaye ofisi katika hizo.

Civil society seeks quick resolution to IEBC row

11th St connector

Monday, July 30, 2012

Kenya police say diplomat is suspect in death of Venezuelan envoy at Nairobi residence

NAIROBI, Kenya (AP) — Kenyan police have asked a court to allow authorities to keep a diplomat in their custody beyond the 24-hour limit as they investigate the murder of the acting Venezuelan ambassador.

A Kenyan police officer leaves the residence of Venezuela’s embassy’s slain charge d’affaires Olga Fonseca at the Runda neighbourhood in Kenya’s capital Nairobi July 27, 2012. REUTERS/Thomas Mukoya

Prosecutor Tabitha Ouya asked the court Monday to grant police 14 days to conclude investigations on Dwight Sagaray, the first secretary at Venezuela’s embassy in Kenya. He is being investigated over the murder of the charge d’affaires and acting ambassador Olga Fonseca. High Court Judge Florence Muchemi said she would rule on the application Tuesday.

Fonseca was found strangled in the embassy’s official residence Friday morning. She reported to Kenya on July 15 to replace former ambassador Gerardo Carillo-Silva.

Carillo-Silva left his posting in Kenya after facing allegations of sexual harassment by the three male workers from the residence.

Copyright 2012 The Associated Press. All rights reserved. This material may not be published, broadcast, rewritten or redistributed.

AFANDE AZIZI MUOGOPE MOLA ZALZALA YA KIAMA NZITO

Na Omar Msangi ‘Annur’

MOJA ya adhkar waliyoleta Waislamu pale Masjid Mbuyuni ni kusoma kipande cha aya ya suratut tiin inayosema: “Alaisallahu biahkamil haakimiina

”Kwamba, “Je, Mwenyezi Mungu si Hakimu muadilifu kuliko mahakimu wote?” Ikiwa na maana kuwa lazima atawalipa watu wote kwa uadilifu kutokana na matendo yao.

Kamanda Azizi Juma Mohamed, amesema kuwa “wafuasi wa Uamsho wakiwa na bendera walianza vurugu, kupanga mawe barabarani na kuchoma moto matairi. Kufuatia hali hiyo, Jeshi la Polisi likaamua kutumia nguvu kuwatawanya kwa mabomu ya machozi na maji yenye kemikali za kuwasha.

”Vyombo vingine vya habari vikadai kuwa Uamsho walianza kuwashambulia Polisi kwa mawe.“Alaisallahu biahkamil haakimiina.” Hapana shaka ipo siku ukweli utadhihiri na kila aliyeumia siku ile ama kupotelewa na kitu, atasimama kudai haki yake.

Yote mpaka kauli hii kwamba Masheikh wa “Uamsho wakiwa na bendera walianza vurugu, kupanga mawe barabarani na kuchoma moto matairi”, itadhihirishwa na kutolewa hukumu na Hakimu Muadilifu. Hiyo ndiyo Siku ambayo vitafunuliwa vitabu ambapo “ utawaona wakosefu wanavyoogopa kwa yale yaliyomo humo (katika vitabu vyao). 

Na watasema: Ole wetu! Kitabu hichi kina nini! Hakiachi dogo wala kubwa ila huliandika? Na watayakuta yote waliyo yatenda yamehudhurishwa hapo. Na Mola wako Mlezi hamdhulumu yeyote.” (18:49). Hata hili la Msikiti wa Mbuyuni nalo limeandikwa? Watahoji na kushangaa waliyoamuru kupiga Waislamu mabomu na wale waliotekeleza amri hiyo. 

“Watasema: Ole wetu! Kitabu hichi kina nini! Hakiachi dogo wala kubwa ila huliandika.” Tunaambiwa Yeye ndiye Mfalme pekee siku hiyo Maalik yaumiddiin. Siku hiyo hatakuwa na nafasi Obama, Kikwete wala Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi. 

Press Briefing by Deputy Press Secretary Josh Earnest

White House Press Briefings are conducted most weekdays from the James S. Brady Press Briefing Room in the West Wing.

Mama Pinda azindua mradi wa maji wa Hospitali ya Mawenzi mjini Moshi leo

  
Mke wa Waziri Mkuu, Mama Tunu Pinda akizindua mradi wa maji katika Hospitali ya Mawenzi pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti anaemaliza Muda wake wa, Richard Wells. Hadi kukamilika kwa mradi huo wa maji safi, Kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Limited imetumia zaidi ya milioni 55 za kitanzania kujenga tanki kubwa la kuhifadhi maji kwa ajili ya matumizi ya hospitali ya Mawenzi mkoani Kilimanjaro.

Mkurugenzi wa Mahusiano na Mawasiliano wa Kampuni ya bia ya Serengeti Bi. Teddy Mapunda, akifafanua juu ya gharama halisi za mradi huo.

“Sisi kampuni ya bia ya Serengeti tunatambua sana changamoto zinazowakabili watanzania, taasisi na mashirika mbalimbali hususani hospitali juu ya upatikanaji wa maji safi na salama, na kwasababu hiyo kampuni ya bia ya Serengeti imeona hilo na kuamua kusadia kutatua tatizo hilo katika maeneo mbalimbali ikianza katika maeneo yanayohitaji huduma ya maji kwa haraka zaidi” alisema Mapunda na kuongeza kuwa kujitolea kusaidia jamii ni moja yab sera za kampuni hiyo kama njia mojawapo ya kurudisha shukrani zake kwa wateja wake na watanzania kwa ujumla.

Mgeni rasmi akifungua maji yanayotoka katika bomba lililounganishwa katika matanki hayo. 
Kwa picha na maelezo zaidi bofya hapa 

13 perish in separate accidents

Traffic officers at Kajjansi examine the car wreckage in which Prisca Mashengyero Tembo was killed. Traffic officers at Kajjansi examine the car wreckage in which Prisca Mashengyero Tembo was killed. PHOTO BY MARTIN SSEBUYIRA

By Martin Ssebuyira 

At least 13 people died, including a minister’s wife in three separate motor accidents that occurred at the weekend. The first accident killed eight family members on Friday night at Papara on Pakwach Road near Murchison Falls National Park as they were heading for burial for one of their relatives.

The deceased, who include Nakasongola Town Council health inspector David Azaga and two army officers died after the driver of a car they were travelling in run into a trailer.

They were laid to rest at Kololo Village in Tara County in Maracha District yesterday. Yesterday, shock gripped residents of Bwebajja after learning that the wife of State Minister for Information Communication Technology George William Nyombi Tembo had been killed in a road accident in head-on-collision at Bwebajja Craft Trading Centre on Entebbe Road on Saturday.

Prisca Mashengyero Tembo, 48, died after her double cabin pick-up rammed into a lorry at around 11:30am. Mr Abdul Kiyimba, a witness, told Daily Monitor yesterday that Mashengyero was coming from Namulundu Medical Centre around Bwebajja and joined Entebbe Road from where a speeding lorry rammed into her car.

WAVUVI WAWILI WALIFARIKI

Vituko vya CCM wilaya ya mjini Zanzibar..!!!

Na Abdallah Vuai

Wiki hii kuna kituko cha aina yake kimetokea ndani ya Chama cha Mapinduzi upande wa Zanzibar kwa wanachama wachache wa Chama hicho Wilaya ya Mjini kuasi dhidi ya mamlaka halali ya CCM. Ni kisa,. 

Kituko kinachoweza kuvunja mbavu pale baadhi ya Wana CCM walipotoa tamko la kuwatuma viongozi wao wa Wilaya kuwataka Makamu Mwemyekiti wa CCM Zanzibar na Rais mstaafu wa Zanzibar,Amani Abeid Karume kunyanganywa kadi kwa madai wamekwenda kinyume na msimamo wa CCM juu ya Muungano.

Viongozi wale waliobariki uasi ndani ya CCM nawawafanisha na aliyekuwa Rais wa Umoja wa Vijana wa African National Congress(ANC) Julius Malema. Katika mkutano huo ambao mbali ya kutaka Makamu Mwenyekiti wao Karume afukuzwe CCM,lakini pia walitaka wanachama wengine kama Mweka Hazina wa Chama hicho Zanzibar,Mansoor Yussuf Himid nae kunyanganywa kadi!

Kisa na mkasa; ni msimamo wa Hamza Hassan Juma, Mshimba Mbarouk, Thuwayba Edington Kisasi, Omar Yussuf Mzee, Mahmoud Mohammed Mussa, Haroun Ali Suleiman, Asha Bakar Makame, Salmin Awadh Salmin, Othman Masoud Othman, Nassor Salim, Mansoor Yussuf Himid katika muundo wa Muungano wakiukosoa hadharani kuwa hauna tija kwa kuwa umeshindwa kufikia kile Wazanzibari walichokuwa wakikitaka baada ya Mapinduzi ya Januari 12,1964 na matumaoni yao katika Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kwa Karume wanamtuhumu kuunga mkono mabadiliko ya muundo wa Muungano, ingawa Karume hajapata kusema aina gani ya mfumo wa muundo wa Muungano anaupendelea.

Man arrested for allegedly planning shooting

Vita vya Aleppo vyapamba moto

Allepo
Mapambano ya kuukamata mji wa Allepo baina ya vikosi vya serikali na waasi yanazidi kupamba moto huko Syria. Waasi sasa wamekiteka kituo muhimu cha ukaguzi kwenye mpaka baina ya nchi hiyo na Uturuki.

Kufuatia hali hiyo, Ufaransa imetangaza kutaka kuitisha kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Waasi wamekitwaa kituo hicho cha Anadan kilichopo kaskazini magharibi mwa mji huo wa Aleppo hii leo baada ya mapigano makali yaliyodumu saa10 mfululizo. Hatua hii inawapa uhuru wa kusafiri kwenye maeneo ya kaskazini na Uturuki.

Shirika la Habari la AFP linaarifu kuwa vifaru saba na magari yenye silaha yamechukuliwa na waasi kutoka vikosi vya serikali, huku mengine manane yakiharibiwa vibaya.

FSA: Mapambano yanaendelea

Wanajeshi sita wameuawa kwenye mapigano hayo na wengine 25 wamekamatwa na kuwekwa kizuizini ambapo waasi wanne pia wameuwa. Kamanda wa Jeshi Huru la Waasi wa Syria, FSA, Khalid al Shamsi anasema kuwa mambo ni mazuri kwa upande wao.

"Hali ni nzuri sana kwetu, tumeuchukua mkoa wa Al Bab na wapiganaji wetu wataendelea kulithibiti jimbo la Aleppo. Sasa tunaimarisha nguvu yetu Aleppo kwa kuwaunganisha wapiganaji wa huko. Tunapata silaha na vifaa kutoka huko na sehemu nyengine za mkoa wa Al Bab". alisema, Kamanda Shamsi.

Romney talks tough on Iran during Israel visit, says Jerusalem to be capital

Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu (R) during his meeting with U.S. Republican presidential candidate Mitt Romney in Jerusalem. (Reuters)
Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu (R) during his meeting with U.S. Republican presidential candidate Mitt Romney in Jerusalem. (Reuters)

By AL ARABIYA WITH AGENCIES

U.S. presidential candidate Mitt Romney presented himself as Israel’s best friend as he spoke aggressively on Sunday about protecting Israel from Iranian nuclear threats and suggested that he was open to breaking with U.S. policy dating to 1967 by moving the United States embassy to Jerusalem if the Israelis asked.

Israel is the second of three stops on an international trip for Romney intended to burnish his foreign policy credentials before he claims the Republican presidential nomination at his party’s national convention in Tampa, Florida, in late August.

While Romney has been highly critical of President Barack Obama’s policy toward Iran and the presumed threat to Israel, he has offered no specifics about how his policy would be substantially different, according to The Associated Press.

But on the issue of the location of the U.S. embassy in Israel, which is in Tel Aviv, Romney told CNN that he thought the U.S. embassy should be moved to Jerusalem if the Israelis make that request. The Israelis have repeatedly sought such a move.

“My understanding is the policy of our nation has been a desire to move our embassy ultimately to the capital (Jerusalem),” he said, adding, “I would only want to do so and to select the timing in accordance with the government of Israel.”

Sikiliza kwa makini Mahojiano na Dr Faustine Ndugulile Part 2

Hii ni sehemu ya pili na ya mwisho ya mahojiano na Mbunge wa Jimbo la Kigamboni (CCM) Dr. Faustine Ndugulile.


Dr. Faustine Ndugulile.

Katika sehemu hii, amezungumzia suala la mgomo wa madaktari na athari zake kwa nchi. Je! Yeye (ambaye pia ni Daktari) anaamini kuwafutia leseni ni uamuzi sahihi?.

Tumesherehekea SIKU YA MASHUJAA NCHINI. Ni kweli kuwa Tanzania TUNA MASHUJAA? TUNAWAENZI VEMA MASHUJAA (kama wapo) na NI VIPI TUNATENGENEZA MASHUJAA WAJAO?

Anazungumzia vipi vipaumbele vya matumizi ya serikali kulingana na mahitaji ya mwananchi?
Ni vipi/ ama kwa kiasi gani kuna ushirikiano wa wabunge (hasa vijana) toka vyama mbalimbali ili kuipeleka Tanzania mbele

Imeelezwa kuwa serikali inachangia 3% ya gharama za mapambano dhidi ya UKIMWI licha ya kuutangaza kama JANGA LA TAIFA. Ni kweli tuna dhamira ya kupambana na ugonjwa huu?
Na upi mwito wake kwa waTanzania wote?

KARIBU

Uganda denies aiding Congo rebel fighters

By John Njoroge

The government has denied reports that it is supporting the M23 rebel group fighting against Kinshasa in the east of the Democratic Republic of Congo.

Congolese flee clashes between M23 rebels and the Congolese army on the edge of Rugari Village, about 37km from Goma in the DR Congo’s restive North Kivu province last week. President Kabila told Congolese state television on Saturday that he had questioned Uganda over it’s alleged support for the rebel M23 movement, and that Kampala had denied any involvement, the AFP news agency reported yesterday. Photo by AFP.

Highly placed sources told Daily Monitorthat President Museveni was in touch with his counterpart, Joseph Kabila, over the matter last week and clarified that Uganda had not taken sides in the matter.

Mr Kabila told Congolese state television on Saturday that he had questioned Uganda over its alleged support for the rebel M23 movement, and that Kampala had denied any involvement, the AFP news agency reported yesterday.

Kabila’s first public comments on the matter came on the same day he sent a special envoy to deliver a message to President Museveni.

Mr Alexander Luba Tembo, DRC’s vice prime minister and Defence minister, delivered the message to President Museveni at his country home in Rwakitura.

A press statement from State House said the two officials “discussed a number of issues of mutual interest between the DRC and Uganda and particularly deliberated on the security situation in Eastern DRC”.

Sources familiar with the matter told Daily Monitor the Congolese special envoy showed evidence of what Kinshasa claims is Rwanda’s support to the M23 rebels.

Gazeti la Mwananchi: CCM,Chadema wawatangazia kiama wabunge mafisadi

DK SLAA AONYA HAKUNA HURUMA, MSEKWA ASEMA RUSHWA ADUI WA HAKI, MBATIA ATOA WIKI MOJA SPIKA AWATAJE WOTE

Kizitto Noya, Dodoma na Leon Bahati, Dar
VYAMA vya CCM na Chadema vimetoa onyo kali kwa wabunge wanaotuhumiwa kwa kashfa ya kuhongwa na baadhi ya kampuni za mafuta na kulihujumu Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), vikisema havitasita kuwawajibisha pindi tuhuma hizo zitakapothibitika.

Kauli ya vyama hivyo imekuja siku moja baada ya wabunge watano, watatu wa CCM na wawili wa upinzani kudaiwa kuhusika na vitendo hivyo vya rushwa, ambavyo vimesababisha Spika wa Bunge, Anne Makinda kuivunja Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini na kuagiza uchunguzi wa kina ufanyike ili majina ya wahusika yawekwe hadharani.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti jana, viongozi wa juu wa vyama hivyo walisema wanasubiri kwa hamu taarifa rasmi kutoka bungeni.

CCM: Rushwa adui wa haki

Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Pius Msekwa alisema chama hicho kimewaapiza wanachama wake wote kutotoa wala kupokea rushwa.

Alisema rushwa ni kosa la jinai hivyo anaamini vyombo husika vya dola vitachukua hatua zinazofaa kwa mujibu wa sheria za nchi.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alikazia kauli hiyo akisema rushwa inaelezwa katika katiba ya chama hicho kwamba ni, ‘adui wa haki’ na wanachama wote waliapishwa kuwa hawatapokea wala kutoa rushwa.

Alisema yeyote anayekwenda kinyume na kanuni za CCM, anajiweka katika kundi la wasaliti wa chama.

Alisema wabunge ni kundi maalumu nchini ambalo linalipwa vizuri ili lisimamie vyema misingi ya maendeleo ya nchi pasipo tamaa wala vishawishi hivyo wanapotajwa miongoni mwa kundi la wala rushwa, CCM kinalaani vikali tukio hilo.

Kuhusu tuhuma hizo kutajwa kuwahusisha wabunge watatu wa chama hicho, Nape aligoma akisema habari hizo siyo rasmi, hivyo hawezi kuzizungumzia.

IEBC tender:Report says all four companies are unsuitable

Ugonjwa wa Ebola wazuka Uganda

Relatives of Ebola patients wait outside the ward, wearing protective masks at Gulu hospital, northern Uganda, Thursday, Oct.19, 2000. Gulu hospital, a sprawling complex of concrete buildings, has been treating 45 people suspected of having the deadly ebola virus, that has so far killed 41 people and possibly infected 70 others. (AP Photo/Sayyid Azim) Maafisa wa afya nchini Uganda wamesema jana Jumamosi (28.07.2012 ) kuwa virusi hatari vya ugonjwa wa Ebola vimesababisha vifo vya watu 14 magharibi mwa nchi hiyo mwezi huu.

Hali hiyo imemaliza wiki kadhaa za kutafakari kuhusu chanzo cha ugonjwa huo wa ajabu ambao umesababisha watu wengi kukimbia makaazi yao.

Maafisa hao pamoja na wawakilishi kutoka shirika la afya ulimwenguni , WHO, wamewaambia waandishi habari mjini Kampala kuwa ugonjwa wa Ebola umezuka nchini Uganda.

Uchunguzi wa maabara uliofanyika katika taasisi ya uchunguzi wa virusi nchini Uganda , umethibitisha kuwa ugonjwa huo hatari ulioripotiwa huko Kibaale kwa hakika ni ugonjwa unaosababisha homa kali na kutokwa na damu wa Ebola, serikali ya Uganda na shirika la WHO zimesema katika taarifa.

Kibaale ni wilaya katika eneo la kati magharibi ya Uganda , ambako watu katika wiki za hivi karibuni wamesumbuliwa na ugonjwa wa ajabu ambao ulikuwa haujulikani unatokea wapi.

Maafisa wa afya nchini Uganda nao pia walikuwa wameshangazwa , na kutumia wiki kadha kufanya uchunguzi katika maabara ambapo hawakupata majibu.

Sunday, July 29, 2012

Sikiliza kwa makini Mahojiano na Mhe. Dr Faustine Ndugulile Part 1


Sehemu ya kwanza kati ya mbili za mahojiano na Mbunge wa Kigamboni (CCM) Dr Faustine Ndugulile ambaye ameeleza mengi kuhusu kongamano kuu la UKIMWI alilohudhuria hapa Washington DC, hali ya mapambano ya UKIMWI nchini Tanzania na pia harakati zake BUNGENI.

Kagusia mgogoro wa MJI MPYA wa KIGAMBONI na mengineyo.
Karibu

Gazeti la NIPASHE Jumapili: Ameir: Kuna harufu chafu CCM Zanzibar

Na Mwinyi Sadallah

Mwanasiasa Mkongwe Zanzibar Ali Ameir Mohamed, amesema wakati umefika kwa viongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi kuwachukulia mapema hatua za kimaadili na kinidhamu wanachama,Wawakilishi na Wabunge wa chama hicho wenye mwelekeo hasi.

Ameir ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa zamani wa CCM Zanzibar na Mbunge wa zamani wa Donge, alisema hayo kupitia mahojiano maalum yaliyofanyika Kijijini kwake huko Donge Mbiji Zanzibar juzi.

Alisema kuwa kuendelea kuwavumilia wanachama wa aina hiyo ni hatari kwa mustakabali wa uhai wa chama hicho akiifananisha hali hiyo ni sawa na mfiwa kufuga maiti ya ndugu yake ndani ya nyumba anayoishi.

“Chama cha siasa ni mkusanyiko wa kundi la watu wanaokubaliana kisera, kiitikadi na kimfumo hivyo anayejitokeza akipingana na masuala hayo hapaswi kubembelezwa au kuonewa muhali”,alisema Ameir ambaye pia amewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Tanzania.

Alisema kiongozi, mwanachama, mbunge au Mwakilishi anayepingana na sera ya msingi ya chama chake analazimika kujitoa ili kuonyesha msimamo wa hisia zake.

Ameir anasema anaamini kuwa taratibu za kikanuni na kikatiba ndani ya chama chake zitafutwa ili kusafisha hewa chafu inayoonekana kutanda.

Kikwete: Agriculture can rid Africa of poverty

President Jakaya Kikwete has reiterated the government’s commitment to increase agricultural production which is the most effective activities to rid the nation out of poverty.

President Jakaya Kikwete

President Kikwete said this during the launch of the Third Convocation of China –Africa Development Partnership against poverty in Dar es Salaam that engagement in agriculture would eradicate poverty in Africa especially South of Sahara.

“Many African governments have not been able to realize agricultural revolution by 100 per cent complicating efforts to eradicate poverty due to financial constraints,” Kikwete said.

Nearly half of the population in Africa, according to him, still lives below the poverty line and pregnant women and children continue to suffer from malnutrition. “Tanzania is determined to fight poverty and has given priority to agriculture to help improve people’s lives.

Implementation of the plan includes mechanization of agriculture through application of modernized technology, improved water services and availability of reliable markets,” President Kikwete said. However, the president made it clear that the success of the government plan to improve agricultural production would depend on availability of funds and technical support, the basic issues that development partners can give serious consideration.

Na Gazeti la NIPASHE: Nahodha awaponda mafisadi wanaopinga Muungano

Na Mwinyi Sadallah

Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Shamsi Vuai Nahodha, amewaponda baadhi ya viongozi wa Zanzibar wanaozungumzia kero na Muungano kwa nia ya kuficha makucha ya ufisadi wao.

Alishusha kombora hilo wakati akichangia hoja kwenye semina ya Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi iliyofanyika juzi mjini hapa.

Alisema kuna ubadhirifu, wizi, uporaji wa ardhi na rasilimali za Zanzibar unaofanywa na baadhi ya vigogo wa Zanzibar lakini vitendo hivyo vinafumbiwa macho.

“Viongozi wanaozungumzia matatizo ya Muungano kwa jazba hapa Zanzibar kwanza wanatakiwa kupima uadilifu na matendo yao ziwemo pia sheria zitakazowabana kujua walipataje mali walizonazo”, alisema

Nahodha ambaye aliwahi kuwa Waziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ) kuanzia mwaka 2000 hadi 2010 kwenye awamu ya Rais Amani Karume alisema hakuna Mtanganyika anayepora ardhi, fedha au kodi za wananchi ila viongozi wa Zanzibar.

Alisema yeye ni muumini wa Muungano wa serikali mbili uliopo na kupendekeza suala la mafuta na gesi asilia litolewa kwenye Muungano kwa kufuata taratibu zilizoliingiza jambo hilo katika orodha ya masuala ya Muungano.

Pia Waziri Nahodha alimuuliza Waziri wa zamani wa SMZ na Serikali ya Muungano Hassan Nassor Moyo kueleza matukio yaliyolitishia usalama wa ndani kuanzia mwaka 1964 hadi 1972.

Ignorant Hostess | All-American Muslim

Hillary jets in to meet Museveni over DR Congo


The US Secretary of State, Hillary Rodham Clinton, is expected in the country on Tuesday, 2, to discuss with President Museveni the worsening security situation in eastern Democratic Republic of Congo, highly-placed sources have confirmed.

A diplomat, who asked not to be named because the secretary’s planned trip is still being kept secret for security reasons, said the two leaders will also discuss the uncertainty surrounding political transition when mandate of the Sheikh Sheriff-led Transitional Federal Government lapses next month.

Ms Elise Crane, the acting public affairs officer at the US Mission in Kampala, said when contacted on Friday: “We have no comment at this point in time.” There is growing unease, according to one senior Uganda government official, among international actors that Somalia could slip into deeper anarchy and AU peacekeepers’ (Amisom) gains on peace restoration reversed, if the expected transition is mismanaged.

The Ugandan military constitutes the largest contingent of Amisom’s 17, 000 troops that has flushed al- Qaeda-affiliated al-Shabaab militants out of the Somali capital, Mogadishu and posted great battlefield successes on their chase in the countrywide.

Michelle Obama alivyobebwa na U.S. Olympic Wrestler Elena Pirozhkova!!


First Lady Michelle Obama alivyo bebwa na mwana Olimpiki wa Marekani, Wrestler Elena Pirozhkova wakati wa aliposalimiana na wanariadhi wa timu ya Marekani katika michezo ya mashindano ya Olimpiki ya mwaka 2012 Summer, wakiwa kwenye Kituo cha Mafunzo ya Olimpiki ya Marekani katika Chuo Kikuu cha East London nchini Uingereza, Julai 27, 2012 . (Picha na Official White House Sonya N. Hebert)

Mkataba Mpya wa Kudhibiti silaha ni lazima uwepo

Silaha mbalimbali zitumikazo katika maeneo ya mapigano.Mkutano unaojadili rasimu ya mkataba mpya wa kudhibiti silaha unamalizika leo ( 27.07.2012) New York, huku mataifa makubwa yakishindwa kufikia maamuzi juu ya mambo muhimu kuhusiana na biashara hiyo ya mabilioni ya dola.

Wakiwa mjini New York, kwa mwezi mmoja sasa washiriki wa mkutano huo wanaonekana kusitasita juu ya orodha ya silaha hizo zitakazojumuishwa katika mkataba huo, unaolenga kuepusha umiliki ovyo wa silaha za kivita, ambazo aghalabu hupoteza maisha ya watu wengi katika nchi zenye mapigano.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon ameeleza masikitiko yake kutokana na maendeleo hafifu ya mkutano huo, unaotegemewa kusiha saa chache zijazo.

Watengenezaji wakubwa wa silaha hizo yaani nchi Ulaya, Marekani, Urusi na China na mataifa yanayoonekana kupinga uundwaji wa mkataba huo mpya kama vile Syria, Korea Kaskazini, Iran, Cuba, Misri na Algeria yanashiriki katika mkutano huo.

Wengi wanaupinga mkataba huu...Kwa nini lakini?

Mwezi Oktoba mwaka 2006, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipiga kura na kuamua kuwepo na mkataba utakaosimamia biashara hii ya shilaha inayokua kwa kasi, ambayo sasa ina thamani ya takriban dola bilioni 60, ambapo Marekani ilipiga kura ya" Hapana".

U.S. sees Israel, tight Mideast ally, as spy threat

U.S. political praise has reached a crescendo ahead of Republican presidential candidate Mitt Romney’s (L) scheduled meeting Sunday with Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu in Jerusalem. (Reuters)
U.S. political praise has reached a crescendo ahead of Republican presidential candidate Mitt Romney’s (L) scheduled meeting Sunday with Israeli Prime Minister Benjamin Netanyahu in Jerusalem. (Reuters)

By THE ASSOCIATED PRESS, WASHINGTON

The CIA station chief opened the locked box containing the sensitive equipment he used from his home in Tel Aviv, Israel, to communicate with CIA headquarters in Virginia, only to find that someone had tampered with it. He sent word to his superiors about the break-in.

The incident, described by three former senior U.S. intelligence officials, might have been dismissed as just another cloak-and-dagger incident in the world of international espionage, except that the same thing had happened to the previous station chief in Israel.

It was a not-so-subtle reminder that, even in a country friendly to the United States, the CIA was itself being watched.

In a separate episode, according to another two former U.S. officials, a CIA officer in Israel came home to find the food in the refrigerator had been rearranged. In all the cases, the U.S. government believes Israel's security services were responsible.

WAISLAMU WAKUTANISHWA NA TAASISI YA ALNNA JAH‏

Sheikh Mkuu wa chuo cha Alnna Jah cha Sheria za kiislam Fahamu Lubwaza kulia akifuturu pamoja na waumini wa Dini ya kiislamu Dar es salaam jana futari hiyo ilikuwa ni moja ya kuitambulisha Taasisi hiyo ya kislamu kwa waislamu kwa ajili ya kuiunga mkono

Sheikh Mkuu wa chuo cha Alnna Jah cha Sheria za kiislam Fahamu Lubwaza kulia akiomba duwa baada ya kufutulu na waislam wenzake Dar es salaam jana futari hiyo ilikuwa ni moja ya kuitambulisha Taasisi hiyo ya kislamu kwa waislamu kwa kuiunga mkono

Baazi ya waumini wa kiislamu wakiomba Duwa baada ya kumaliza kufuturu wakati wa kuitambulisha Sheikh Mkuu wa chuo cha Alnna Jah cha Sheria za kiislam (Picha zote na Majira)

East Africa moves to curb cyber crimes

By JAMES GASHUMBA, EANA

East Africa is fast-tracking the implementation of joint initiatives to combat the rising challenge of cyber crimes that threaten peace and stability in the region.

Dr Bitange Ndemo. Photo/Nation

Government officials say the region is vulnerable to a range of online criminal activities, including financial fraud, drugs human trafficking, and terrorism. “There is need to develop a common platform to address cyber security. As a region, we must begin to cooperate to deal with cyber threats atNational and regional levels,” Kenya’s Permanent Secretary in the Information Ministry Dr Bitange Ndemo said at an East African Internet Governance Forum in Nairobi, Kenya.

Kenya has scaled up efforts to combat cyber crimes through a multi-stakeholder approach involving the government, industry and civil society organizations. “Kenya has a national cyber security steering committee hosted by the Communications Commission of Kenya (CCK), law enforcement agencies and industry players are part of this initiative,” Ndemo said.

He regretted cyber crimes have significantly reversed gains made by higher internet penetration in Kenya. The country has taken a lead role in galvanising regional efforts to fight cyber crimes. According to Ndemo, a cyber security management task force chaired by Kenya has been coordinating activities aimed at curbing cyber crimes in the five East African Community member states.

Neno La Leo: Na Wabunge Wetu Wengine Ni Wezi, hakyamungu!

Ndugu zangu,

Waziri Muhongo ameusema ukweli wake kule Dodoma. Nami nimefuatilia sinema hii ya Dodoma, kila inavyoendelea ndivyo ninavyozidi kuchoka. Ama hakika, tunakokwenda siko, tuna lazima ya kujipanga upya.

Namsifu Waziri Muhongo kwa ujasiri wake. Amutusaidia sana kuyajua yale ambayo yangetuchukua muda mrefu kuyajua. Kwa kusimama kwenye ukweli Waziri Muhungo ameitendea haki nchi yetu tuliyozaliwa.

Na tulipofikia hapa ni ukweli tu ndio utakaotusaidia kutupa ahueni ya hali mbaya tuliyonayo kama taifa. Huu si wakati wa kutanguliza siasa za vyama bali kuitanguliza Nchi yetu tuliyozaliwa na tunayoipenda. Kutanguliza uzalendo.

Leo tunabaki vinywa wazi kusikia kuwa hata wachungaji, na wengine wamejiingiza Bungeni, kuwa nao wanawaibia Watanzania wenzao. Kwamba nao hawatosheki. Wanaiba huku wakitaja neno la Mungu. Leo hata wale wanaojinadi kuwa ni watetezi wa wanyonge wameanza kutiliwa mashaka. Uwezo wao wa kiuchumi unahusianishwa na ' madudu' kama haya ya Tanesco. Na kuna hata wenye ' kuwafuturisha' wenzao wenye uwezo kwa fedha walizowaibia wananchi wanyonge. Hawa hawana cha swaumu bali wanashinda na njaa kwa dhambi ya wizi wao.

Tuna lazima sasa ya kuamka na kuwabana wezi wetu. Mwizi ni mwizi tu, hata kama ni mheshimiwa Mbunge.Na ukweli ndio unaohitajika sasa. Na si nusu ukweli, bali ukweli mzima hata kama utatugharimu maisha yetu.

Sherehe ya wana jumuia wa DMV

Saturday, July 28, 2012

Press Briefing

White House Press Briefings are conducted most weekdays from the James S. Brady Press Briefing Room in the West Wing.

Mchungaji Amani Golugwa ahudhuria Mkutano wa kimataifa wa UKIMWI (AIDS 2012) Washington DC


Mwenyekiti wa tawi la Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Washington DC Mh. Cosmas Wambura, akiwa na Katibu wa chama cha Chadema mkoani Arusha Mchungaji Amani Golugwa, walipohudhuria katika Mkutano wa kimataifa wa UKIMWI (AIDS 2012) Washington DC uliomalizika rasmi jana Ijumaa Aug, 27 Convention Center Washington DC.

Baadhi ya watu kutoka mataifa mbali mbali wakimiminika kwenye jumba la Convention Center, mahali ulipofanyika mkutano huo wa XIX International AIDS Conference (AIDS 2012) Washington D.C. 

XIX International AIDS Conference (AIDS 2012) Washington D.C.      Closing Session    Former United States President William Clinton        © IAS/Ryan Rayburn - Commercialimage.net
Rais wa zamani  Bill Clinton akitoa hotuba ya kufunga  rasmi Mkutano wa Kimataifa wa UKIMWI uliofanyika kwa masiku kadha ndani ya  mjini  Washington, DC siku ya Ijumaa Aug 27, 2012 ambapo mataifa malimbali yalijumuika katika kupiga vita ugonjwa sugu duniani HIV.

Ratiba ya futari ya pamoja Washington DC

RAIS JAKAYA KIKWETE AZINDUA KARAKANA (HANGA) YA NDEGE ZA SHIRIKA LA NDEGE LA PRECISION AIR


Mwenyekiti wa bodi ya Shirika la ndege la Precision Air Bw. Michael Shirima akimkabidhi zawadi Mh Rais Dk. Jakaya Kikwete mara baada ya kuzinduz rasmi karakana na ndege za shirika hili (Hanga) kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere leo jijini Dar es salaam, Karakana hiyo itakuwa na ikihudumia ndege za shirika hilo la mashirika mengine pia lakini pia itapokea wanafunzi walio kwenye mafunzo ya Uinjini wa ndege kutoka katika vuo vya ndani.

Rais Jakaya Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe pamoja na wakuu mbalimbali wa shirika la ndege la Precision Air na wafanyakazi wa shirika hilo mara baada ya uzinduzi wa (Hanga) hiyo

Rais Jakaya Kikwete akiweka mkasi mara baada ya kukata utepe ikiwa ni ishara ya uzinduzi wa Karakana na ndege za shirika la ndege la Precision Air leo kwenye uwanja wa ndege wa Mwalimu J.K.Nyerere jijini Dar es salaam kulia ni Bw Bw. Michael Shirima. Kwapich a zaidi bofya hapa 

Weekly Address: The House of Representatives Must Act on Middle Class Tax Cut Extension

President Obama urges Republicans in the House of Representatives to act on his proposal to protect middle class families and small businesses from being hit with a big tax hike next year.

UPDF sends 3,200 more troops to Somalia

The army has passed out a new battalion comprising of 3,237 specially trained troops for deployment against the al Qaeda-linked al-Shabaab terrorists in the war-torn Somalia.


UPDF soldiers from Battle Group 10 carry out military exercises during a pass out ceremony at Singo

This will be Uganda’s 10th battle group to be deployed in Somalia since the inception of the African Union (AU) peacekeeping mission (AMISOM) in 2007.

The battle group 10 will replace battle group eight that will return home upon their arrival in Mogadishu.

The troops, who completed a four-month course at Singo military centre in Nakaseke district on Friday, comprise of British and French trained snipers equipped with distinct martial skills.

Other foreign trainers came from the Africa Contingency Operations Training and Assistance (ACOTA), which comprises of mainly retired UN servicemen and women.

Passing out the team on Friday, Maj. Gen. Levy Karuhanga, the UPDF commander of reserve forces, and a group of senior officers were mesmerized by the antics of cordon and search as well as shooting exhibited by the graduands, especially snipers.

“The skills demonstrated imply you are ready to take up the mandate. It’s a manifestation of the maturity needed to pursue terrorists and restore calm among the Somalis which had been denied to them by the al-Shabaab,” said Karuhanga.

MULTICHOICE TANZANIA YAFUTURISHA WANAHABARI KATIKA HAFLA YA KUKARIBISHA MICHUANO YA OLYMPICS.‏

Meneja Uhusiano wa Kampuni ya Multichoice Tanzania Barbara Kambogi akizungumza na waandishi wa habari kwenye hafla ya futari wakati wa kukaribisha michuano ya Olympics iliyofanyika kwenye hoteli ya New Africa jijini Dar.

Barbara Kambogi ametumia fursa hiyo pia kuwataarifu Watanzania kuwa Kampuni yao pendwa ya Multichoice kupitia king'amuzi chao cha DStv inawaletea chaneli maalum itakayokuwa ikuzungumzia maadili ya Uislam katika kipindi hichi cha mfungo wa Ramadan ambacho pamoja na kuwakumbusha wakubwa pia tutawaelimisha watoto kujua nini wanapaswa kufanya ndani ya Uislam.

Amesema gharama za kufunga king'amuzi zimeshushwa na kufikia shilingi 169,000 ambapo atakayejiunganisha atafurahia chaneli nane za Super Sport zitakazokuwa zikonyesha michezo ya Omlympics iliyoanza jijini London kwa muda wa saa 24.

Pia amewakumbusha Watanzania wasisahau kua Kagame Cup iko live kupitia chaneli ya Super Sport 9 ya DStv.

Baadhi ya Waandishi habari kutoka vyombo mbalimbali nchini waliohudhuria hafla hiyo wakijisevia Futari.

Waandishi wa habari wakienjoy futari iliyoandaliwa na kampuni ya Multichoice Tanzania. picha zaidi bofya hapa.

U.N. arms talks end without deal, U.S. blamed for deadlock

A mock graveyard set up by the Control Arms coalition next to the United Nations building in New York. One person every minute dies from armed violence around the world. (Reuters)
A mock graveyard set up by the Control Arms coalition next to the United Nations building in New York. One person every minute dies from armed violence around the world. (Reuters)

By AL ARABIYA WITH AGENCIES

U.N. negotiations to draft the first international treaty on the multi-billion-dollar arms trade have ended without a deal, with some diplomats blaming the United States for the deadlock.

More than 170 countries have spent the past month in New York negotiating a treaty, which needed to be adopted by consensus, so any one country effectively could have vetoed a deal. Instead, no decision was taken on a draft treaty.

But this leaves the door open for further talks and a draft arms-trade treaty could be brought to the 193-nation U.N. General Assembly and adopted with a two-thirds majority vote. Diplomats said there could be a vote by the end of the year.

“We feel that we could have agreed (a treaty). It is disappointing that more time is needed. But an arms-trade treaty is coming - not today - but soon. We’ve taken a big step forward,” said a spokesman for Britain’s delegation.

One person every minute dies from armed violence around the world, and arms control activists say a convention is needed to prevent illicitly traded guns from pouring into conflict zones and fueling wars and atrocities. They cited conflicts in Syria and elsewhere as examples of why a treaty is necessary.

Tume ya kukusanya maoni ya Katiba yaendelea kukusanya maoni

Bi. Aziza Juma (27), mkazi wa Wilaya ya Kishapu, mkaoni Shinyanga akitoa akitoa maoni yake kuhusu Katiba Mpya kwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba ilipofanya mkutano kijijini hapo jana (Alhamisi, Julai 26, 2012)

Wananchi wa Kijiji cha Maganzo, Kata ya Songwa, Wilayani Kishapu mkoani Shinyanga wakifuatilia mkutano wa kukusanya maoni ya wananchi kuhusu Katiba Mpya jana (Alhamisi, Julai 26, 2012)

Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba katika picha ya kumbukumbu na wanafunzi wa Shule ya Msingi Michungwani iliyopo kijiji cha michungwani, Kata ya Segera wilayani Handeni mkoani Tanga mara baada ya mkutano wa kukusanya maoni kuhusu Katiba Mpya.