Kati kati ni balozi wa Tanzania Marekani na Mexico Mwanaidi Sinare Maajar kulia kwake Rais wa Jumuiya ya watanzania Washington Dc Iddy Sandaly na kushoto ni Bw. Oswald Urassa(CFO) wa Tanzania Mortgage Refinance Co.Ltd(TMRC).
Wana DMV wakisikiliza kwa makini maelezo ya ukopeshaji mikopo ya nyumba.Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) Nehemiah Mchechu pamoja na mkurugenzi mkuu wa TMRC (Tanzania Mortgage Refinance Company) na Mkurugenzi Mkuu Azania Bank, pamoja na Maofisa wa benk mbali mbali.walipokuwa na Jumuia ya waTanzania waishio DMV siku ya Ijumaa June 1, 2012 kwenye ukumbi wa Mirage Hall, wakizungumzia utaratibu mzima wa suala la mikopo ya nyumba (Tanzania Mortgage Refinance Company)
Katika mkutano huo wa uwekezaji, Tanzania Mortgage Refinance Co.Ltd(TMRC), walipata fursa ya kuwaeleza utaratibu mzima wa maisha ni nyumba, pamoja na kujijibu maswali mbali mbali yalioulizwa na wana Jumuia ya Watanzania waishio hapa na kuelimisha zaidi katika mkutano huo ili nae Mtanzania aliekuwepo njee ya nchi kufaidika zaidi kwa mradi huo wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC)
Sikiliza kwa makini Audio ya Mkutano uliofanyika siku ya Ijumaa June 1, 2012 kwenye ukumbi wa Mirage Hall uliopo University Bld, Hysattsville, Maryland Nchini Marekani, (Audio na swahilivilla.blogspot.com)



Kaka ebou shatry kazi nzuri sana yani nakushukulu kwa uweo wako kwa wote niko Boston na nilikwa na fuatilia sana matangazo yako, na hii uliotuwekea redio umekamilisha uweleo wangu juu ya Tanzania Mortgage Refinance yani jamanii keep it up we love you baby
ReplyDelete