Makamo wa kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe Seif Shariff atakuwa na ziara ya siku chache hapa UK.
Jumuiya Zanzibar Welfare Association UK kwa kushirikiana na Ubalozi wa Tanzania hapa UK inapenda kuwaalika kila mmoja wenu kwenu mkutano wa Hadhara utakaofanyika siku ya Ijumaa saa kumi na mbili jioni kwenye Ukumbi wa University of London Union, Malet Street, London, WC1E 7HY.
Kwa wale ambao watakuwa na shauku ya kumuuliza masuala basi hii ndio nafasi ya kuweza kufanya hivyo.
Vile vile kutokana na upungufu wa nafasi za kuegeshea magari, tunawanasihi kila atakae bahatika kufika hapo kutumia usafiri ambao hautawalazimu kutafuta nafasi za kuegeshea magari yao.



No comments:
Post a Comment