If you need it, we can provide: • USA 24 hours Passport service • Rush and emergency USA passport • Expedited Visa process for U.S. & foreign countries • Document Authentication •Document Legalization..For more information please contact us at: 703-286-7713

http://swahilivilla.blogspot.com/2014/01/mahojiano-na-faria-zam-kuhusu-msaada-wa.htmlKwa kuchangia chochote kile alichonacho kupitia Hilmy Disability Charity Organisation. Wasiliana na Mkurugezi wa Hilmy Disability Charity Organisation. Faria Zam. kwa UK Number ya Simu. 745-501-4372 Au Abou Shatry. U.S.A No' 301-728-3977

 http://www.dickysmallsauto.com/

DICK SMALLS AUTO MOTIVE WE CAN HANDLE ALL OF YOUR REPAIR AND SERVICE NEEDS INCLUDING CALL US NOW!(301) 931-3300. 10111B BACOCON DRIVE,BELTSVILLE,MD 20705


Sunday, November 18, 2012

Kampuni ya Export Trading Group yawafikiria wakulima Zanzibar

Kampuni inayojishughulisha na Biashara za nje yenye Makao Makuu yake Mjini Dar es salaam {Export Trading Group} ina mpango wa kuisaidia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika kuwajengea uwezo wakulima kumudu kuzalisha Kitaalamu ili kufikia kiwango cha uwezo wa kuuza mazao yao nje ya Nchi.

Mwenyekiti wa Kampuni ya Biashara za Nje ya Mjini Dar es salaam { ETG } Bwana Mahesh Patel akizungumza na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hapo Nyumbani kwake Mazizini Nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Mwenyekiti wa Kampuni hiyo Bwana Mahesh Patel alieleza hayo wakati wa mazungumzo yake na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi yaliyofanyika nyumbani kwa Balozi Seif Mazizini Nje Kidogo ya Mji wa Zanzibar.

Mwenyekiti huyo wa Export Trading Group Bwana Mahesh Patel alisema Kampuni yake imeshajipangia utaratibu wa namna ya kusaidia wakulima katika kuwapatia taaluma ya kisasa ya uzalishaji wa mazao yao.

Alisema utaratibu huo tayari unaendelea kutolewa na Kampuni yake katika Mataifa mbali mbali Barani Afrika na hivi sasa wameona ipo haja kwa Uongozi wa kampuni hiyo kutoa upendeleo pia kwa wakulima wa Zanzibar.

“ Tumekuwa tukiunga mkono juhudi za wakulima katika kuwapatia Taaluma bora za kisasa ambazo tayari zinafanya kazi katika Nchi kadhaa zikiwemo Malawi, Zambia, Zimbabwe,Burundi na Rwanda”. Alisisitiza Bwana Patel.

“ Taaluma hiyo ilienga zaidi katika mazao ya Ufuta, Mahindi zikiwemo pia mashine za kisasa za kubambulia Korosho katika Mkoa wa Tanga”. Aliendelea kufafanua Mwenyekiti huyo wa ETG.

Bwana Mahesh Patel alieleza kwamba katika kusaidia wakulima wa Zanzibar kimapato ili kumudu vyema kuendesha Maisha yao ameiomba Serikali kufikiria namna ya kuipatia Kampuni yake uwezekano wa kuzalisha Bidhaa ya Sukari hapa Nchini.


Alisema kuendelezwa kwa sekta hiyo Nchini upo uwezekano mkubwa wa kuongeza ajira kwa wakulima walaio wengi kumudu kuendesha Ukulima wa Miwa na hatimae kuiuza kiwandani baada ya kupatiwa Taaluma sahihi.

Naye Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi aliipongeza Kampuni hiyo inayojishughulisha na Biashara za Nje { ETG } kwa uamuzi wake wa kusaidia nguvu za wakulima Kitaalamu katika uzalishaji mali.

Balozi Seif alisema Kilimo bado kinaendelea kuwa uti wa Mgongo wa Taifa hili lakini kinachokosekana zaidi hivi sasa kwa wakulima walio wengi ni ufinyu wa Taaluma ya kuendesha kilimo hicho.

“ Tumekuwa tukishuhudia mfano wa wakulima wetu wengi wa mpunga wamekuwa wakilima zao hilo muhimu katika eneo kubwa lakini kipato chake hakilingani na nguvu na uwezo waliotumia katika uzalishaji”. Alifafanua Balozi Seif.

Alisema upo uwezekano wa wakulima wengi kufaidika na kilimo cha miwa na baadaye kuiuza kiwandani ambacho utafiti unaonyesha kwamba mapato yake ni makubwa ikilinganishwa na kilimo cha Mpunga kilichozoeleka kwa wakulima hao.

Kampuni ya Biashara za Nje { ETG} inaendelea kutoa huduma kwa Mataifa kumi na nane Barani Afrika Pamoja na India, China na Kusini Mashariki mwa Bara la Asia tokea kuundwa kwake Mwaka 1967.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako