If you need it, we can provide: • USA 24 hours Passport service • Rush and emergency USA passport • Expedited Visa process for U.S. & foreign countries • Document Authentication •Document Legalization..For more information please contact us at: 703-286-7713

http://swahilivilla.blogspot.com/2014/01/mahojiano-na-faria-zam-kuhusu-msaada-wa.htmlKwa kuchangia chochote kile alichonacho kupitia Hilmy Disability Charity Organisation. Wasiliana na Mkurugezi wa Hilmy Disability Charity Organisation. Faria Zam. kwa UK Number ya Simu. 745-501-4372 Au Abou Shatry. U.S.A No' 301-728-3977

 http://www.dickysmallsauto.com/

DICK SMALLS AUTO MOTIVE WE CAN HANDLE ALL OF YOUR REPAIR AND SERVICE NEEDS INCLUDING CALL US NOW!(301) 931-3300. 10111B BACOCON DRIVE,BELTSVILLE,MD 20705


Sunday, December 2, 2012

NI WAKATI WA KUANZISHA SHULE ZA MICHEZO - MH. LOWASSA

WAZIRI Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli Mh. Edward Lowassa amewashauri wabunge wa timu ya Bunge Sports kufikiri juu ya kutunga sera ya michezo itakayoruhusu kuanzishwa kwa Shule za Michezo (Sports Academy) hapa nchini.

Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Jimbo la Monduli,Mh. Edward Lowassa (wa pili kushoto)

Lowassa ameyasema hayo jana,baada ya kuialika nyumbani kwake timu hiyo iliyopiga kambi ya jijini Arusha tayari kwa mashindano ya Mabunge ya Afrika Mashariki jijini Nairobi.

“Nilisikitika kweli Timu ya Taifa ya Kilimanjaro Stars ilipofungwa na Burundi kwenye mchezo wa pili wa Mashindano ya CECAFA huni Uganda, pamoja na juhudi za Rais Jakaya Kikwete kuleta makocha bado tumefungwa na Burundi iliyotoka kwenye vita juzi!.

“Nyinyi ni watunga Sera, ni wachezaji mnajua changamoto zinazofanya tusifike juu, umefika wakati wa kuwa na Shule za Michezo zinazotambuliwa na Sera zetu.

“Mpira ni chakula cha Watanzania, wanapenda mpira sana. Napendekeza baada ya kurejea anzeni kufikiria juu ya kutunga Sera ya kuwa na Shule za Michezo. Kipingu amejitahidi kuwa na kitu kama hiki lakini amebakia peke yake hakuna anayemuunga mkono,” alisema Lowassa.

Alisema kuwapo kwa Timu ya Bunge Sports kutasaidia kufikiria juu ya mafanikio ya mchezo wa mpira wa miguu, pete na michezo mingine.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Amos Makalla aliyeongozana na timu hiyo alimwambia Mh. Lowassa kwamba serikali ipo katika hatua za mwisho za kukamilisha Sera za michezo.


“Sera na sheria za sasa za michezo kweli haziendani kabisa na wakat,zote ni za zamani. Serikali imejipanga kuzifanyia kazi.

“Changamoto uliyoitoa ya kuanzisha Shule za Michezo na kuendeleza michezo nchini tunaipokea na tutaifanyia kazi.

“Nilipoteuliwa kuwa Naibu Waziri kwenye Wizara hii niliwaambia watu na binafsi namshukuru Rais Kikwete, kwamba upele ulipata mkunaji kwani mimi ni mwanamichezo na uwanjani ni kiungo mchezeshaji,” alisema Makala.

Naye Mwenyekiti wa Timu hiyo ya Bunge Sports inayoundwa na wabunge kutoka Baraza la Wawakilishi na Bunge la Jamhuri, Iddi Azan alimshukuru Mh. Lowassa kwa mawazo yake na kuahidi kuyafanyia kazi.

“Kwanza tunaahidi ushindi kwa nchi, Bunge letu na haya uliyoyasema tunaahidi kuendelea kuyafanyia kazi kwani tunatambua sheria na Sera za michezo zimepitwa na wakati,” alisema Azan.

Timu hiyo ya Bunge Sports ilikuwa na wachezaji wake wote waliopo kwenye kambi jijini Arusha wanaounda timu ya Mpira wa miguu na Pete.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako