If you need it, we can provide: • USA 24 hours Passport service • Rush and emergency USA passport • Expedited Visa process for U.S. & foreign countries • Document Authentication •Document Legalization..For more information please contact us at: 703-286-7713

http://swahilivilla.blogspot.com/2014/01/mahojiano-na-faria-zam-kuhusu-msaada-wa.htmlKwa kuchangia chochote kile alichonacho kupitia Hilmy Disability Charity Organisation. Wasiliana na Mkurugezi wa Hilmy Disability Charity Organisation. Faria Zam. kwa UK Number ya Simu. 745-501-4372 Au Abou Shatry. U.S.A No' 301-728-3977

 http://www.dickysmallsauto.com/

DICK SMALLS AUTO MOTIVE WE CAN HANDLE ALL OF YOUR REPAIR AND SERVICE NEEDS INCLUDING CALL US NOW!(301) 931-3300. 10111B BACOCON DRIVE,BELTSVILLE,MD 20705


Wednesday, March 20, 2013

Marekani yajiandaa kumsafirisha Bosco Ntaganda Hague

Na Victor Melkizedeck Abuso

Marekani inasema Ubalozi wake mjini Kigali nchini Rwanda unajiandaa kumsafirisha Jenerali Bosco Ntaganda aliyejisalimisha kwenye ubalozi wake na kwamba wana matumaini kupata ushirikiano toka kwa serikali ya Rwanda.

Bosco Ntaganda has been wanted by the ICC since 2006
Bosco Ntagannda

Bosco Ntaganda aliishangaza dunia juma hili baada ya kujisalimisha mwenyewe kwenye ubalozi wa Marekani nchini Rwanda akitaka msaada wa kufikishwa kwenye Mahakama ya Kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC.

Msemaji wa kundi la M 23 linalowakilishwa na Askofu Jean Marie Runiga, Salomon Baravuga amesema kiongozi wake ndiye aliyemshawishi Ntaganda kujisalimisha huku akikanusha kundi lake kuwa na uhusiano na kiongozi huyo.

Kwa upande mwingine msemaji wa kisiasa wa kundi la M23 linaloongozwa na Sultan makenga, Betrand Bisimwa ameendelea kusisitiza kuwa Runiga na kundi lake walikuwa na uhusiano wa karibu na Ntaganda waliyetaka arejee katika kundi lao.

Rais Joseph Kabila ameendelea kukutana na viongozi mbalimbali nchini humo kujadili hali ya amani Mashariki mwa nchi hiyo huku baada ya Ntaganda kujisalimisha.

Ntaganda anatuhumiwa kuongoza makundi kadhaa ya uasi Mashariki mwa nchi hiyo kabla ya kupewa cheo katika jeshi la serikali kaa njiamojawapo ya kuleta amani Mashariki mwa nchi hiyo.


Aidha, ametuhumiwa kuongoza kundi la waasi la M 23 kulipa silaha ili kukabiliana na serikali ya Kinsasha huku akitihumiwa na Mahakama ya ICC kutekeleza visa vya ukiuwkaji wa haki za bindamu ikiwemo kuwaajiri watoto wadogo katika jeshi lake na pia kutekeleza mauji na ubakaji wa wanawake.

Ofisi ya kiongozi wa Mashtaka katika Mahakama ya Kimataifa ya ICC mjini Hague imesema kuwa inawasiliana na serikali ya Rwanda pamoja na Marekani kuhakikisha kuwa Ntaganda anafika Hague ili kufunguliwa mashtaka yanayomkabili.

Mahakama hiyo ya ICC imeongeza kuwa kujisalimisha kwa Ntaganda ni habari njema kwa raia wote wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambao wameteseka mikononi mwa kiongozi huyo wa kundi la waasi.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako