Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itashiriki katika mkutano wa Geneva 2 kwa ajili ya kuutafutia ufumbuzi mgogoro wa Syria lakini bila masharti yoyote.
Huku akiashiria mwaliko wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa Iran wa kushiriki mkutano huo, Marzie Afkham amesema, ingawa inaunga mkono kutatuliwa kwa njia za kisiasa mgogoro wa Syria lakini Tehran haikubali masharti na kwamba Iran ni miongoni mwa nchi za mwanzo zilizosisitiza kuwa mazungumzo ndiyo njia pekee ya kutatuliwa mgogoro huo.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran aidha amesema, mkutano wa Geneva 2 unaweza kuandaa mazingira mazuri kwa ajili ya kuchukuliwa hatua zinazofaa zinatakazowezesha kutatuliwa mgogoro wa Syria.
Hayo yanajiri huku kundi la wapinzani wa Syria la SNC likitishia kuwa, halitashiriki mkutano huo utakaofanyika Januari 22 iwapo Iran pia itashiriki.
Via kiswahili.irib.ir
Via kiswahili.irib.ir




KICHWA CHA HABARI KINGINE NA HABARI NYINGINE VP? SLAA NA SYRIA WAP NA WAPI?
ReplyDelete