Serikali ya Sudan Kusini imetangaza kuwa, kujiunga nchi hiyo na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu kunahitajia maoni ya wananchi na kuitishwa kura ya maoni.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Sudan Kusini Barnaba Marial Benjamin ameeleza kuwa, suala la Sudan Kusini kuwa mwanachama wa jumuiya ya Arab League litaamuliwa na wananchi wa nchi hiyo.
Ameongeza kuwa, uhusiano wa serikali ya Juba na nchi zote za Kiarabu ni madhubuti na mzuri.
Katika upande mwingine, mazungumzo kati ya pande hasimu za Sudan Kusini yaliyoanza karibu miezi 10 iliyopita yamesimama.
Michael Makuei mkuu wa timu ya mazungumzo ya serikali ya Sudan Kusini amesema mazungumzo hayo yamesimama lakini yataanza tena Oktoba 16.
Ameongeza kuwa, uamuzi huo umechukuliwa ili kila upande upate fursa ya kujadili masuala muhimu kuhusiana na mazungumzo hayo, hasa nafasi ya waziri mkuu na iwapo rais atakuwa mkuu wa nchi pamoja na serikali au la.
Chanzo: kiswahili.irib.ir




No comments:
Post a Comment