If you need it, we can provide: • USA 24 hours Passport service • Rush and emergency USA passport • Expedited Visa process for U.S. & foreign countries • Document Authentication •Document Legalization..For more information please contact us at: 703-286-7713

http://swahilivilla.blogspot.com/2014/01/mahojiano-na-faria-zam-kuhusu-msaada-wa.htmlKwa kuchangia chochote kile alichonacho kupitia Hilmy Disability Charity Organisation. Wasiliana na Mkurugezi wa Hilmy Disability Charity Organisation. Faria Zam. kwa UK Number ya Simu. 745-501-4372 Au Abou Shatry. U.S.A No' 301-728-3977

 http://www.dickysmallsauto.com/

DICK SMALLS AUTO MOTIVE WE CAN HANDLE ALL OF YOUR REPAIR AND SERVICE NEEDS INCLUDING CALL US NOW!(301) 931-3300. 10111B BACOCON DRIVE,BELTSVILLE,MD 20705


Tuesday, October 7, 2014

Wapiganaji wa IS waendelea kudhibiti baadi ya maeneo ya Kobane

Raia huyu  wa kikurdi aangalia mapigano katika mji wa Kobane akiwa katika kijiji chaMursitpinar, kwenye mpaka wa Uturuki na Syria, Oktoba 6 mwaka 2014.
Raia huyu wa kikurdi aangalia mapigano 
katika mji wa Kobane akiwa katika kijiji cha
Mursitpinar, kwenye mpaka wa Uturuki na
Syria, Oktoba 6 mwaka 2014.
AFP PHOTO / ARIS MESSINIS
Na RFI

Siku moja baada ya wapiganaji wa Dola la Kiislam kudhibiti maeneo matatu mashariki mwa Kobane nchini Syria, mapigano yanaendela kurindima mashariki na kusini mwa mji huo karibu na mpaka wa Syria na Uturuki.

Kwa mujibu wa shirika la haki za binadamu nchini Syria, muungano wa kimataifa umeendesha usiku wa jumatatu kuamkia leo jumanne mashambulizi mapya dhidi ya ngome za wapiganaji wa dola la Kiislam.

Ni wiki tatu sasa tangu mapigano kati ya wapiganaji wa Dola la Kiislam na wapiganaji wa Kiikurdi kuzuka karibu na mpaka wa Syria na Uturuki. Wapiganaji wa dola la Kiislam wametishia kuudhbiti mji wa Kobane.

Kwa mujibu wa kiongozi wa shirika la kutetea haki zabinadamu nchini syria, mapigano hayo kati ya wapiganaji wa Dola la Kiislam na wapiganaji wa kikurdi yameelekea kuwa mashambulizi ya kuvizia kwenye barabara za mji wa Kobane. Raia wameyahama makaazi yao na kukimbilia katika nchi jirani ya Uturuki. Kobane ni mji wa tatu unaokaliwa na watu kutoka jamii ya wakurdi wa Syria.


Hayo yakijiri, Bunge la Uturuki liliiruhusu Alhamisi serikali ya Ankara kuchukua uamzi wa kutuma majeshi yake nchini Syria na Iraq kwa lengo la kuendesha mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa dola la Kiislam.

Barani Ulaya, kumekua na uhamasishaji wa haraka na wenye nguvu, hususan katika nchi za Ufaransa, ujerumani, Ubelgiji, Uholanzi. Denmark na Norway. Viwanja vya ndege vimefungwa, huku maandamano yakipangwa kufanyika ili kushinikiza mataifa hayo kupambana vilivyo kwa kuhofia kutekwa kwa mji wa Kobane na wapiganaji wa Dola la Kiislam.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako