If you need it, we can provide: • USA 24 hours Passport service • Rush and emergency USA passport • Expedited Visa process for U.S. & foreign countries • Document Authentication •Document Legalization..For more information please contact us at: 703-286-7713

http://swahilivilla.blogspot.com/2014/01/mahojiano-na-faria-zam-kuhusu-msaada-wa.htmlKwa kuchangia chochote kile alichonacho kupitia Hilmy Disability Charity Organisation. Wasiliana na Mkurugezi wa Hilmy Disability Charity Organisation. Faria Zam. kwa UK Number ya Simu. 745-501-4372 Au Abou Shatry. U.S.A No' 301-728-3977

 http://www.dickysmallsauto.com/

DICK SMALLS AUTO MOTIVE WE CAN HANDLE ALL OF YOUR REPAIR AND SERVICE NEEDS INCLUDING CALL US NOW!(301) 931-3300. 10111B BACOCON DRIVE,BELTSVILLE,MD 20705


Showing posts with label Bouteflika kunga'atuka mamlakani. Show all posts
Showing posts with label Bouteflika kunga'atuka mamlakani. Show all posts

Tuesday, April 2, 2019

Bouteflika kunga'atuka mamlakani

Mwandishi: Lilian Mtono. Mhariri: Bruce Amani

Rais wa Algeria Abdelaziz Bouteflika ataachia wadhifa wake huo Aprili 28, kabla ya kumalizika kwa muhula wake wa nne. Ameamua kuchukua hatua hiyo baada ya washirika wake wa karibu kujitenga naye

Algerien, Algier: Algerisches Militär fordert Absetzung von Präsident Bouteflika (picture alliance/dpa)
Ni hatua ambayo imechukuliwa katika wakati ambapo pia kuna maandamano makubwa ya raia ya kumshinikiza kiongozi huyo mdhaifu kung'atuka.

Bouteflika mwenye umri wa miaka 82, ambaye pia amekuwa akionekana mara chache hadharani tangu alipopatwa na kiharusi mnamo mwaka 2013, amekuwa akikabiliwa na wakati mgumu mamlakani, kutokana na kuongezeka kwa shinikizo kwa wiki kadhaa baada ya jaribio lake la kutaka kusalia madarakani baada ya miaka 20 ya utawala.

Bila ya kutoa maelezo zaidi, taarifa kutoka ofisi ya rais imesema Bouteflika atajiuzulu kabla ya Aprili 28, baada ya kuchukuliwa kwa kile kilichotajwa kama "maamuzi muhimu".

Hata hivyo, taarifa iliyotolewa na shirika rasmi la habari nchini humo la APS imesema Bouteflika atachukua kwanza hatua zinazolenga kuhakikisha taasisi za serikali zinaendelea kufanya kazi zake katika kipindi cha mpito.

Rais wa chama cha upinzani cha UCP Zoubida Assoul amezungumzia hatua hiyo ya rais Bouteflika, kwenye mahojiano na shirika la habari la AFP. Alisema "Sitaki kumsubiri hadi atangaze kujiuzulu kwa sababu tunajua kwamba anatakiwa kuondoka mamlakani ifikapo Aprili 28. Kwa hiyo sio tukio la kushangaza na wala halikutangazwa kwetu kama kitu kikubwa. Tungependa atuambie anarejea kwenye mkakati wake uliokataliwa na watu na hata upinzani, ikiwa ni pamoja na mimi."

Algerien Protest gegen Präsident Abdelaziz Bouteflika in Algiers (Reuters/R. Boudina)
Maandamano yalihanikiza katika jiji la Algiers kumpinga Bouteflika

Katika siku za karibuni, Algeria imekumbwa na maandamano makubwa hasa baada ya rais kutangaza mnamo mwezi Februari kwamba angegombea awamu ya tano ya urais. Bouteflika alisema mwezi uliopita kwamba angejiondoa kwenye kinyang'anyiro cha urais na kuuahirisha hadi mwezi huu wa Aprili, hatua iliyowaongezea ghadhabu waadamanaji, walioichukulia hatua hiyo kama mbinu ya kuongeza muda wa kusalia mamlakani.

Bado kuna wasiwasi wa mabadiliko iwapo mfumo uleule utasalia baada ya kuondoka Bouteflika.

Maoni yako