Kamati ya Bunge ya Haki na Maadili imewasilisha Bungeni Hoja ya kulitaka Bunge hilo kusitisha kufanya kazi na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG) Profesa Mussa Assad, kutokana na kauli yake ya kuliita Bunge hilo dhaifu...
Wabunge wamechangia hoja na kutoa maoni yao kuhusiana na hoja hiyo ambapo wanakinzana pande moja inakubaliana na hoja huku pande nyingine ikikataa na kudai kuwa CAG hana kosa lolote.
Wabunge wa Upinzani wamechukizwa na hoja hiyo na kuamua kutoka nje ya ukumbi wa Bunge.


